Header Ads

BRELA:TULIISAJILI KENERL LTD

Na Happiness Katabazi

MSAJILI Msaidizi Mwandamizi wa BRELA, Maria Kiwia(52) ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kwamba kampuni ya Kenerl Ltd iliyodaiwa ni kampuni hewa na ilichota sh bilioni sita katika Benki Kuu ya Tanzania, ni kampuni halili kwani imesajiliwa na BRELA kwa mujibu wa taratibu zote za kisheria.


Kiwia ambaye ni mwanasheria kitaaluma alieleza alieleza hayo jana wakati akihojiwa na wakili wa utetezi Alex Mgongolwa na wakili wa serikali Timon Vitalis mbele ya jopo mahakimu wakazi, Prophil Lyimo, Edson Mkasimongwa na Salome Mwandu, alipokuwa akitoa ushahidi wake katika kesi hiyo.

Shahidi huyo ambaye mwaka 2000 alikuwa akifanyakazi katika Kitengo cha Msajili wa Makampuni akiwa na wadhifa huo,shughuli zake zilikuwa ni kusimamia usajili wa makampuni na kutoa ushauri na alama za biashara na kuongeza kuwa anaifahamu vyema kampuni hiyo ya Kenerl Ltd kwani ilisajiliwa na Msajili wa Makampuni na kwamba yeye ndiye aliyeuska na ubadilishwaji wa jina la biashara ya kampuni hiyo ambayo awali ilikuwa ikiitwa Kenerl Mills Holdings Ltd kwenda Kenerl Ltd.

“Naitambua kampuni hiyo kwani ilisajiliwa na BRELA na mimi ndiye niliyeshughulikia na ombi lao kubadilisha jina la biashara na kuisajili hivyo si sahihi kusema kampuni hii ni hewa....kampuni hii ipo hai na ilitimiza matakwa yote ndiyo maana ikasajiliwa na hata siku moja BRELA haijawahi kulalamika kwamba kampuni hiyo ilikiuka taratibu za usajili”alidai Kiwia ambaye kwasasa ni wakili katika Benki ya Dimond Trust.

Kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi aliarisha usikilizaji wa kesi hiyo Mei 21-25 mwaka huu, na akauamuru upande wa mashitaka uakikishe siku hiyo unaleta mashahidi bila kukosa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Aprili 23 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.