Header Ads

KWA HERI KAMANDA KONGA,TUTAKUKUMBUKA DAIMA


Na Happiness Katabazi

APRILI 5 mwaka huu, saa 10:12 jioni nikiwa ofisi nilipokuwa katika chumba chetu cha habari nilipokea simu toka kwa mama yangu mzazi Oliva Katabazi ikiniarifu kwamba kaka yangu Aristariko Konga (49) amefariki dunia.

Na akaniambia hanitanii kwamba taarifa hizo ni za kweli na yeye amepigiwa simu na mke wa marehemu, Aniwiye Konga ambaye ndiye alikuwa akimuuguza katika Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi Lugalo Dar es Salaam kwa takribani wiki tatu sasa.

Baada ya kupokea taarifa hizo za kusikitisha,nilijikuta nikipaza sauti kwa uchungu ndani ya chumba chetu habari cha gazeti hili kwamba ‘Konga amefariki’ na waandishi wenzangu waliokuwepo ofisi Kulwa Karedia, Betty Kangonga,Martin Malela na Meneja Uhusiano wa Benki ya NMB Shy-Rose Banji ambaye siku hiyo ya Jumatatu ya Pasaka, alifika ofisini kwetu kikazi walinizunguka kwa simanzi na mkuu wangu wa kazi Kulwa Karedia aliniambia pamoja na kupokea simu hiyo alinitaka niandike habari ya kifo cha mwandishi huyo mkongwe.

Nami nilifanya hivyo nilikaa kwenye Kompyuta nakuanza kuandika habari huku nikilengwa na machozi ila kwasababu nisizozifahamu habari hiyo iliyotakiwa itoke kwenye gazeti Tanzania Daima la jana, haikutoka.

Mara ya mwisho mimi kuzungumza kwa simu na Konga ilikuwa ni siku ya Sikuu ya Pasaka April 4 mwaka huu, ambapo niliipiga simu yake akapokea mke wake nikasalimiana nae akaniambia kaka yangu Konga hali yake imebadilika hata kuzungumza sauti haitoki vizuri lakini akaniambia ngoja ajaribu kumpa simu ndipo nikazungumza naye huku sauti yake nikiisikia kwa taabu akaniambia kwamba hajisikii vizuri hata kuzungumza anazungumza kwa tabu namini nikamtakia Pasaka njema na kumuadi kesho yake ambayo ndiyo siku aliyokufa ningeenda tena kumuona.Uzuni Konga amekwenda.

Kisha nikatuma ujumbe mfupi kwa ofisa mwandamizi mmoja toka ofisi moja nyeti serikalini na kumueleza hali ya Konga siyo nzuri naye akasema kesho yake angeenda kumuuona na kweli ofisa huyo wa serikali Jumatatu ya Pasaka majira ya saa sita mchana alikwenda kumuona Konga wodini na alipomaliza kumuona aliniarifu Konga hazungumzi tena na hali yake ni mbaya kilichobaki tumuombee kwa mungu.Nilisikitika sana.

Huyu mtumishi wa serikali (jina na mhifadhi) ndiye alikuwa mtu wa kwanza kabisa mwanzoni mwa Februali mwaka huu, kunitumia ujumbe mfupi kuniarifu kwamba alikuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,kikazi akamkuta mwandishi mmoja wa gazeti la Mwanahalisi yaani Konga anaumwa vibaya na akanitaka nipeleleze afya yake inaendeleaje.

Mimi nilimjibu Konga namfahamu ni kaka yangu kiumri na amenitangulia kwenye fani hii ya Uandishi wa Habari,nilichokifanya Februali mwaka huu, nikawa nampigia mara kwa mara simu mhariri wa Michezo wa Gazeti la Mwanahalisi Alfred Lucas kumuuliza kama Konga anaumwa na alinijibu ni kweli anaumwa na kwamba yeye amekuwa akiagizwa mara kwa mara na uongozi wa ofisi yake kwenda kumjulia hali nyumbani kwa Konga na kumjulia hali pamoja na kutoa msaada uliokuwa ukiitajika.

Nakumbuka Lucas alieleza kwamba Konga ni mgonjwa na nikamtaka Alfred anipatie namba ya simu ya Konga, alifanya hivyo alinipatia nami kwa zaidi ya wiki tatu nikiipiga namba ile ya mtandao wa Tigo, simu ile ikawa haipatikani mwisho nikamweleza Alfred mbona ile simu uliyonipatia haipatikani, akanieleza amesikia kwamba Konga amebadili simu amekuwa na mtandao wa Vodacome ila namba hiyo anayo Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Mseto na Mwanahalisi Saed Kubenea akaniaidi kumwomba anipatie.

Nilisubiri bila mafanikio, nikaamua kumpatia maendeleo ya nilipofikia yule ofisa mwandamizi wa serikali na kumweleza kwamba namba ya Konga nimeshindwa kuipata akanijibu kupitia ujumbe mfupi, ‘sawa’.

Kesho yake yaani Machi 18 mwaka huu, ofisa yule wa serikali aliangaika na akaakikisha anaipata namba hiyo ya Konga na akanitumia na akasema anachokitaka kwangu ni kuakisha Konga anatibiwa na anatolewa ndani ya nyumba kwa nguvu na anaopelekewa Hospitali akatibiwe kwani kwa uchunguzi alioufanya na amejiridhisha kwamba Konga halikuwa haendi hospitali kupata matibabu.

Baada ya hapo nilimpigia simu Konga akapokea nikajitambulisha kwake akafurahi sana nikamueleza kwamba nimesikia kwamba anaumwa, akanijibu ni kweli nikamuuliza anatibiwa hopsitali gani akaniambia anatibiwa hospitali ya Mikocheni kwa Dk.Kairuki ,kwakuwa nilikuwa najua ananidanganya hatibiwi kokote, nikamweleza kwanini asiende kutibiwa katika hospitali ya Lugalo, akanijibu hana mtu anayefahamu pale nikamweleza kwamba hospitali ya Lugalo haina urasimu na wananchi wa kada zote wanaruhusiwa kutibiwa pale na kama yupo tayari aseme kesho mke wake ampeleke pale hospitali.

Konga ambaye ni mwandishi wa habari mkongwe na mchambuzi wa masuala ya siasa ,jamii na utawala, alinijibu kwa unyenyekevu, atashukuru sana kama nitafanya hivyo na nikamwambia kesho yake saa kumi usiku ya siku ya Ijumaa Machi 19 mwaka huu,nilimpigia simu Konga ili kuakikisha je ni kweli atakwenda Lugalo siku hiyo kutibiwa, lakini simu ilipokelewa na mkewe namini nikajitambulisha akasema mumewe alikuwa amemweleza jana yake na mkewe akasema ndiyo anaenda kutafuta gari la kukodi ili ampeleke Lugalo na kunieleza kwamba usiku kucha hawakulala kwasababu alizidiwa sana.

Baada ya mkewe kuniakikishia kwamba wangekwenda Lugalo, saa kumi mbili kasorobo asubuhi ya siku hiyo nilimpigia Kubenea na Alfred kwa bahati mbaya simu zao zilikuwa zimezimwa.Ndipo muda huo nikaamua kumpigia simu Mshauri wa habari wa gazeti la Mwanahalisi ambaye pia ni mwandishi wa habari mkongwe nchini Ndimara Tigambwage kuwaeleza nilivyofanya jitihada zangu hizo.

Ndimara akaniunga mkono na kusema hilo ni la msingi ni vyema Konga akafie hospitali na siyo nyumbani ila akasema yeye hana mamlaka ya utawala katika Mwanahalisi ila akanisii sana nisubiri kupambazuke uenda simu ya Alfed na Kubenea zitakuwa zimewashwa na atawaeleza yote ili uongozi wa kampuni huo une unaweza kusaidia nini.

Lakini ilipofika saa mbili asubuhi ya siku hiyo mkewe alinipigia simu akinieleza kwamba Konga amekataa kutoka ndani na amesema hataki kupelekwa hospitali nikamweleza mke wake akaa atulie pale nyumbani kwake, nitampa jibu baada ya muda mchache.Ndipo Ndimara alinipigia simu akinieleza kwamba ameishazungumza na Kubenea na kwamba Kubenea ametoa maelekezo kwa Mhariri wake Alfred Lucas kuhusu kumsaidia .Uzuni Konga amekwenda.

Na nikamweleza Ndimara licha amenieleza hayo lakini mkewe amenipigia simu akiniambia kwamba mumewe hataki kwenda hospitali na ndipo nilipomueleza tena Ndimara kwamba amueleze Alfred Lucas akifika nyumbani kwa Konga pale Ubungo Kibo asifanye majadiliano naye ambambe amtumbukize kwenye gari na kisha ampeleke Lugalo akatibiwe.Uzuni Konga amekwenda.

Ilipofika majira ya saa tatu asubuhi ya siku hiyo tena , Alfred alinipigia na kuniambia tayari wameishamwingiza kwa nguvu Konga kwenye gari na wapo njiani wanaelekea kuelekea Lugalo ila hali ya Konga ni mbaya sana.

Siku hiyo walipofika Lugalo pale mapokezi baahati nzuri walipokelewa na ofisa wa JWTZ mwenye cheo cha Kepteni ambaye Dk.Hashim Thabit ambaye alimpatia matibabu ya awali na kumuandikia alazwe na alienda kulazwa wodi Na.11 na baadaye akaamishiwa wodi 11C ambapo alilazwa hapo hadi umauti ulipomkuta juzi.

Kufikia kwa hatua hiyo tena nilitumua ujumbe mfupi kwa yule ofisa wa serikali na kumweleza kwamba hatimaye Konga ameishafikishwa Lugalo na amelazwa. Na yule ofisa nakumbuka alinijibu kupitia ujumbe mfupi akiniambia yafuatayo:

“Nashukuru sana.Wapo watu wanaogopa sana hospitali hata kuwatizama wagonjwa wanaogopa.Wewe kweli nimeamini ni mpiganaji .Unaweza uongozi”

Kwa wale tuliopata fursa ya kumtembelea mara kadhaa Konga akiwa wodi, ndani ya siku mbili tangu afikishwe hopitalini pale ambapo alifikishwa akiwa hajifahamu wala hamtambui mtu, alianza kupata nafuu na kuzinduka na kuanza kufahamu watu na kujua kwamba yupo hospitali.

Lakini wakati harakati zote zinafanyika hadi anafishwa hopitalini hapo alikuwa hazitambui na baada ya siku ya tatu kupata fahamu yaani siku ya tatu kupata fahamu Machi 17 mwaka huu, nilikwenda pale wodini na kumwelezea mkanda mzima mbele ya mke wake aliinuka na kunishukuru na kushukuru wote waliofanya jitihada za kumfikisha pale na kusema atatuombea kwa mungu.

Minilimweleza yeye ni binadamu mwenzetu hivyo hakukuwa na maana yoyote kumuacha aendelee kutaabika bila kumpatia msaada uliopo ndani ya uwezo wetu na kwamba yote ni mipango ya mungu.

Kutoka kutojifahamu alipata nafuu anakaanza kula chakula, na kutoka wodi kwenda kukaa kwenye baraza za hospitalini hapo na kuzungumza na watu lakini hali yake ya kiafya ilianza kudorola Ijumaa Kuu ya wiki iliyopita ambapo hata chakula alikuwa hataki kula na ndipo juzi asubuhi ndugu zake walipoamua kumuandaa kiroho na kumletea mchungaji ambaye alimuongoza kusali sara ya toba na hatimaye juzi saa tisa alivyopelekwa bafuni na mkewe kuoga ndipo alipofariki bafuni wakati amekaa kwenye kiti hospitalini hapo.Uzuni Konga amekwenda jamani.

Konga amefariki ameacha watoto wawili na mke mmoja.Amekufa wakati uhuru wa wananchi wa kujieleza na kutoa maoni yao bila kubudhiwa na vyombo vya dola unazidi kukuwa chini ya serikali ya awamu ya nne.

Konga umetutoka wakati bado taifa lilikuwa likitaji mchango wako wa kwa njia ya kalamu katika kuliletea maendeleo taifa letu.Konga umekufa kindi hiki wakati taaluma ya habari imeingiliwa na mdudu rushwa na miongoni mwetu tumegeuka kuwa manyang’au wa kuwa na tamaa ya fedha na mali, tumekuwa na makundi na tumekubali kutumiwa vibaya na wanasiasa,baadhi ya wanabahari wamepakatwa na wanasiasa na matokeo yake wamekuwa wakiandika habari na makala za uchonganishi baina ya wanasiasa ambazo hazileti tija kwa taifa letu.

Konga umekufa wakati nchi yetu Oktoba mwaka huu, inaingia kwenye uchaguzi mkuu ,mchango wako wa makala za siasa ulikuwa ukiitajika sana.Mwili wa marehemu ilitorowa heshima za mwisho jana katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Ubungo-Gide na kuudhuriwa na waandishi wa habari wa kongwe na chipukizi nchini na jioni mwili wake ulisafirishwa kwenda nyumbani kwao wilayani Makete mkoani Iringa kwaajili ya mazishi.Uzuni Konga amekwenda.

Mazuri yaliyofanywa na Konga enzi za uhai wake naahidi nitayaenzi na mabaya yaliyofanywa nae kama binadamu hatutayaenzi.Shukurani za pekee ziwaendee madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Jeshi Ulinzi la Wananchi Lugalo, kwa jitihada zao za kitabu walizozitoa kwa mpendwa wetu Konga ili kuokoa maisha yake hadi siku alipikumbwa na umauti.

Konga ana historia pana kwenye tasnia ya habari hapa nchini lakini hadi umauti ulikuwa mwandishi wa habari wa mwandamizi wa gazeti la Mwanahalisi, lakini amepata mwandishi na Mhariri Mwandamizi wa kampuni zinzozochapisha magazeti ya Mwananchi, Raia Mwema,The Guradian na iliyokuwa Habari Corporation ambayo kwasasa ina tambulika kwa jina la New Habari.

Konga atakumbukwa kwa ujasiri wake katika kusimamia mambo ya msingi kwani wakarti fulani mwanzo mwa mwaka 2000 aliunguliwa nyumba katika mazingira yaliyoacha utata mwingi suala ambalo lilidhaniwa kuwa uunguaji huo ulikuwa ni shambulio la kulipiza kisasi dhidi ya msimamo wa habari na makala alizokuwa akiandika katika masuala kadhaa ya kitaifa.

Sisi tulimpenda Konga lakini Mungu amempenda zaidi.Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.Uzuni Konga amekwenda.

0716 774494
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, April 8 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.