Header Ads

LIYUMBA APANGUA SHITAKA KUU


Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana ilimfutia shitaka moja kati ya mashitaka mawili yaliyokuwa yakimkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba, kwa maelezo kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kupeleka ushahidi wa kuthibitisha shitaka mojawapo.


Katika kesi hiyo ya jiani Na.105/2009 inayomkabili mshitakiwa huyo, Liyumba alikuwa akikabiliwa na shitaka la matumuzi mabaya ya ofisi ya umma pale alipoidhinisha ujenzi wa mradi wa majengo ya minara pacha “Twin Tower” bila idhini ya Bodi ya Wakurugenzi. Shitaka la pili ni kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221.

Uamuzi huo ulitolewa jana na kiongozi wa Jopo la Mahakimu Wakazi, Edson Mkasimongwa, aliyekuwa akisaidiana na Lameck Mlacha na Benedict Mwingwa. Jana kesi hiyo jana ambayo iliudhuriwa na umati wa watu wakiwemo ndugu na jamaa wa mshitakiwa kwaajili ya mahakama hiyo kutoa uamuzi wa kwamba mshitakiwa huyo ana kesi ya kujibu au la.

Akisoma uamuzi huo uliochukua dakika 50 na huku akionyesha kujiamini Mkasimogwa alisema jopo hilo limepitia kwa kina ushahidi uliotolewa na mashahidi nane wa upande wa Jamhuri na vielelezo 12 na kupitia majumuisho ya kesi hiyo yaliyowasilisha na mawakili wa pande zote mbili, jopo hilo limeona Liyumba ana kesi ya kujibu katika shitaka la kwanza la matumuzi mabaya ya ofisi ya umma. Amefutiwa shitaka la pili la kusababisha hasara.

Mkasomongwa ambaye alikuwa akisoma uamuzi huo huku akionyesha umakini alisema kwa mujibu wa ushahidi uliotelewa umedhibitisha kwamba ofisi ya Kurugenzi ya Utumishi na Utawala ilikuwa ikiongozwa na Liyumba na ndiyo ofisi iliyokuwa imepewa jukumu la kuradi mradi huo wa ujenzi licha hakuna ushahidi uliotolewa mahakamani kwamba mshitakiwa huyo alikuwa na mamlaka ya kuidhinisha mabadiliko ya ujenzi wa mradi wa majengo hayo isipokuwa.

“Na kwamba mujibu wa ushahidi huo umeonyesha Meneja Mradi sisi tunamkewa Meneja mradi chini ya Liyumba kwani alikuwa akiripoti kwa mshitakiwa na mshitakiwa alikuwa akiripoti kwenye Menejimenti na Menejimenti ilikuwa ikiripoti kwenye bodi kuhusu taarifa ya maendeleo ya mradi …sasa kwa mtiririko huo tunaungana na upande wa mashitaka mabadiliko ya ongezeko la mradi kabla ya kufanyika yalipaswa yapewe idhini na bodi na si kama ilivyodaiwa kufanywa na Menejimenti kufanyamabadiliko ya mradi na kisha kupeleka taarifa kwa bodi ili ipewe idhini.

“Kwa mujibu wa kielelezo cha kwanza ambacho kilikuwa ni mkataba, hakukuwa na mkataba mwingine mradi ule ulikuwa na thamani ya dola za Kimarekani milioni 73,600 lakini katika utekelezaji ambapo Liyumba alikuwa akisimamia gharama zilipanda na kufikia dola 357,675 na zilitumika na ushahidi unaonyesha mradi huu menejimenti ilipitisha ongezeko hilo awali kabla idhini ya bodi.

“Pia kuna ushahidi kwamba masula hayo ya mabadiliko ya mradi hayakujadiliwa na Menejimenti ya Benki isipokuwa Bodi ndiyo iliyoyajadili, na inaonekana ni matumuzi ya bodi; hivyo mahakama inamuona mshitakiwa anapaswa ajitetee au ajieleze kuhusu shitaka la kwanza,” alisema Mkasimongwa.

Kuhusu shitaka la pili la kusababisha hasara, alisema mahakama ilipaswa ielezwe na upande wa mashitaka kuwa mshitakiwa alisababisha hasara kwa makusudi, au bahati mbaya na kuendelea kuchambua kuwa kuhusu hoja ya serikali kupata hasara, mwajiri wa mshitakiwa alipaswa aonyeshe mradi uligharimu kiasi ghani na hasara iliyopatikana ni kiasi gani.

Akichambua ushahidi wa shahidi wa nane ambaye ni Naibu Gavana wa Benki Kuu, Juma Reli, ambaye aliieleza mahakama hiyo kuwa anashindwa kuthibitishia mahakama hasara iliyopatikana kwasababu hadi sasa ripoti ya mwisho ya fedha za matumuzi ya ujenzi wa mradi huo haijatoka, alisema kutokana na ushahidi huo umesababishia mahakama ifikie uamuzi wa kujiridhisha kwamba ushahidi ushahidi wa upande wa mashitaka una mkanganyiko.

“Mahakama inaamini alichokizungumza Juma Reli ni ukweli mtu na ndiyo maana alivyomaliza kutoa ushahidi wake alitoka ndani ya mahakama hii kwa amani na mawakili wa serikali hakulalamika kwamba shahidi wao hametoa ushahidi wa uongo…kwahiyo mahakama hii inatamka kiasi cha fedha kilichoongezeka katika ujenzi wa mradi ule kilitumika kwa utaratibu wa fedha za serikali zinavyotakiwa zitumike.

“Kwa heshima na taadhima jopo hili halikubaliani na hoja ya upande wa mashitaka iliyotaka mahakama hiyo isikubaliane na hoja ya upande wa utetezi iliyosema huwezi kuthibitisha hasara katika mradi huo hadi uwe na ripoti ya mwisho ya fedha zilizotumika kwenye mradi ule kwasababu hata ripoti hiyo ingekuwepo isingeweza kuondoa makadirio ya gharama zilizokadiwa na mkadiriaji wa majengo wa mradi huo.

“Mahakama inasisitiza haikubaliani na hoja hiyo ya upande wa mashitaka kwasababu katika kesi hiyo hasara iliyodaiwa amepata mwajiri wa mshitakiwa ni lazima ithibitishwe kwa namba na ripoti…sasa katika kesi hii hasara iliyopatikana haiwezi kuwa sawa na namba ya ripoti ya Mkadiriaji wa Majengo kwani majengo ya nyongeza yamejengwa …labda ingekuwa majengo hayo mengine yanayodaiwa kujengwa nje ya mkataba wa awali na fedha hazionekana hilo lingekuwa ni jambo jingine.

“Na upande wa mashitaka wenywe kupitia mawakili wake ukiri mbele yetu kwamba makadirio ya awali yaliyapaswa kujengwa magorofa 14 lakini baada ya mabadiliko ya ongezeko la ujenzi ziliongezeka ghorofa tatu nyingine juu hivyo kufanya kuwa na majengo mawili na kila jingo lina ghorofa 17 kwenda juu na kweli majengo yamejengwa …na kwa maelezo hayo mahakama hii inamfutia mshitakiwa shitaka la pili kwa mujibu wa kifungu cha 230 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 an na akaueleza upande wa mashitaka upo huru kukata rufaa kama haujalidhika na uamuzi huo.‘alisema Mkasimongwa na kusababisha ndugu na jamaa wa mshitakiwa wakisika kwa sauti wakisema, ‘Asante Yesu.’”

Baada ya hakimu huyo kumaliza hukumu hiyo wakili wa utetezi Majura Magafu, Onesmo Kyauke, Hudson Ndusyepo na Jaji Mstaafu Hillary Mkate pamoja na wakili wa serikali Prosper Mwangamila na Ben Lincoln na Tabu Mzee walisema hawana pingamizi na uamuzi huo.

Wakili Magafu alidai kuwa mahakama hiyo imefuta shtaka hilo ambali linaangukia kifungu cha 148(5)(e)cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ambayo ndiyo iliyotumika kumpatia dhamana awali mshitakiwa na ilimtaka atoe fedha taslimu au hati ya mali yenye thamani ya sh bilioni 110 na mshitakiwa alishindwa kutimiza masharti hayo, hivyo akaomba mahakama itoe masharti mapya ya dhamana yanayoendana na shitaka la kwanza ambalo ni la matumuzi mabaya ya ofisi ya umma ambalo aliangukii kwenye matakwa ya kifungu hicho.

Alipotakiwa na mahakama hiyo aseme chochote kuhusu ombi hilo lilowasilisha na utetezi, wakili wa seriakali Mwangamila alisema hawana pingamizi na ombi hilo ila aliomba mahakama itoe masharti ya dhamana yatakayofanya mshitakiwa aweze kufika mahakamani.

Akisoma uamuzi uamuzi wa ombi hilo la kutaka jopo hilo litoe masharti mapya ya dhamana kwa mashitakiwa huyo Hakimu Mkazi Lameck Mlacha kwaniaba ya jopo alisema wamepata wasaa wakupitia uamuzi dhamana uliotolewa na Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ,Geofrey Shahidi mwaka jana, alisema jopo limejikuta halipo tayari kukubaliana maombi ya pande hizo hizo mbili kwasababu mahakama ya Hakimu Mkazi haina mamlaka ya kutengua uamuzi huo wa mahakama kuu ambao ulimpatia masharti ya dhamana mshitakiwa huyo chini ya kifungu cha 148(5)(e) cha Sheria ya Makosa ya Jinai, ila kama mshitakiwa anataka kupewa dhamana basi aende kuomba Mahakama Kuu.

“Jopo hili limeona busara kesi hiyo imefikia uamuzi wa juu sana kwa hiyo si vyema leo tuendelee kuzungumzia maombi ya dhamana ya mshitakiwa hivyo tunaona ni vyema kesi hii ikaendelea kusikilizwa,” alisema Hakimu Mkazi Mlacha na kusababisha ndugu wa mshitakiwa na kuyeyusha matumaini ya ndugu yao angepata dhamana.

Aidha Magafu aliomba amri zilizokwisha tolewa na mahakama zibaki kama zilivyo na akasema ni mapema wao kueleza kwamba wataka rufaa mahakama kuu na kuongeza kuwa mshitakiwa wake atatoa ushahidi wake kwa kiapo na anakusudia kuleta mashahidi sita na vilelezo ila kwana hakuwa katika nafasi nzuri ya kuweza kutaja orodha ya mashahidi hao na kuomba apewe wiki moja ili aweze kuleta orodha hiyo ya mashahidi.

Hakimu Mkazi Edson Mkasimongwa aliamuru upande wa utetezi April 16 mwaka huu, upande wa utetezi ulete orodha ya mashahidi wake mahakamani na iwapatie orodha hiyo upande wa mashitaka na kisha anairisha kesi hiyo hadi April 22 na 23 mwaka huu, ambapo Liyumba atajitetea na mashahidi wake watatoa ushahidi.

Hata hivyo saa tisa Alasiri jana wakili wa Liyumba, Onesmo Kyauke aliwasilisha barua katika uongozi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili iweze kuwapatia nakala ya mwenendo wa uamuzi ulitolewa na jopo hilo jana ili waweze kupitia kwa kina uamuzi huo na kisha wajue nini cha kufanya.

Januari 27, mwaka jana, Liyumba na Meneja Mradi wa Benki Kuu, Deogratius Kweka, walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na kusomewa mashitaka hayo ya kuidhinisha mradi wa majengo ya minara pacha bila idhini ya bodi ya wakurugenzi na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221.

Mei 27 mwaka jana, mahakama hiyo iliwafutia kesi, lakini muda mfupi baada ya kuachiliwa walikamatwa tena mahakamani hapo na Mei 28 mwaka jana, Liyumba peke yake ndiye aliyerudishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka hayo na Kweka akawa ameachiliwa huru. Tangu kipindi hicho hadi sasa Liyumba anaendelea kusota rumande, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana, ambapo mahakama ilimtaka atoe fedha taslimu au hati ya mali yenye thamani ya sh bilioni 11.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, April 10 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.