Header Ads

KARATA YA MWISHO BABU SEYA

Na Happiness Katabazi

MWANAMUZIKI mahiri wa muziki wa dansi nchini Nguza Vikings “Babu Seya na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha” jana walirusha karata yao ya mwisho katika Mahakama ya Rufaa Tanzania wakiomba mahakama hiyo ipitie upya hukumu iliyotolewa mahakama hiyo ambayo ilisisitiza kwamba warufani hao waendelee kutumikia kifungo cha maisha jela.


Ombi hilo liliwasilishwa jana na mawakili wa warufani hao Mabere Marando na Gabiel Mnyere na kwa mujibu wa nakala ya ombi hilo warufani wanaomba mahakama hiyo ya rufaa ipitie upya hukumu iliyotolewa Februali mwaka huu na majaji wa tatu wa mahakama hiyo kwani walipitiwa kisheria kutoa hukumu ile.

“Wanaamini mahakama hii ikipitia upya hukumu iliyotolewa na majaji wa mahakama hiyo watabaini mapungufu yaliyofanywa na majaji wale watatu na kisha watafutia adhabu ya kifungo cha maisha washitakiwa hao”alisema Marando.

Babu Seya na mwanawake wanatumikia kifungo cha maisha jela baada ya mahakama ya Hakimu MKazi Kisutu, Mahakama Kuu na Mahakama hiyo ya rufaa kuwakuta na hatia ya kubaka watoto wa shule.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi,Aprili 10 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.