Header Ads

LIYUMBA KUANZA KUJITETEA

Na Happiness Katabazi

ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye anakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi ya umma, kwa kuidhinisha ujenzi wa mradi wa majengo ya minara pacha ‘Twin Towers’ bila idhini ya bodi ya wakurugenzi, ataanza kujitetea wiki ijayo.


Kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Edson Mkasimangwa, alisema jana kuwa Liyumba ataanza kujitetea Aprili 22 na 23.

Awali, wakili wa mshitakiwa huyo, Majura Magafu, alidai mteja wake anatarajia kuwa na mashahidi watatu katika utetezi wake.

Aliwataja mashahidi hao kuwa ni Mkurugenzi wa Mahesebu wa BoT, Rashid Mwanga, Kaimu Katibu wa Kitengo cha Sheria BoT, aliyekuwa Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi wa BoT, anakabiliwa na kesi mbili za Akaunti ya Maeni ya Nje (EPA) ambaye mpaka sasa anasota rumande kwa kushindwa kutumiza masharti ya dhamana, Bosco Kimela, Mkurugenzi wa Fedha Mstaafu wa BoT, Elisa Isangya.

Kimela na Isanya, awali walikuwa mashahdi wa upande wa mashitaka, lakini baadaye waliondolewa kwenye orodha ya mashahidi wa upande huo.

Wakili Magafu baada ya kutaja shahidi hao aliiomba mahakama kutoa hati za kuitwa mahakamani kwa mashahidi hao.

Wakili huyo aliwasilisha orodha hiyo ya mashahidi kutokana na amri iliyotolewa na kiongozi wa jopo la mahakimu wakazi wakiongozwa na Mkasimangwa Aprili 9 mwaka huu.

Aprili 9, Mahakama ya Kisutu ilimfutia Liyumba shitaka moja la kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221, hivyo kubakiwa na shitaka moja la matumizi mabaya ya ofisi ya umma.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Aprili 17 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.