Header Ads

MBATIA ALIPA DHAMANA MIL.9/-

Na Happiness Katabazi
HATIMAYE aliyekuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chama cha (NCCR)-Mageuzi, James Mbatia atekeleza amri ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kwa vitendo, iliyomtaka alipe shilingi milioni tisa kama dhamana ya kesi ya kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 dhidi ya mbunge wa sasa wa jimbo hilo kwa tiketi ya (Chadema) , Halima Mdee kuwa ndiye mbunge alishinda.

Wakili wa walalamikaji hao watatu yaani Mbatia na wapiga kula wake Hemed Manoni na Solomoni Mfunda, Mohamed Tibanyendera aliliambia Tanzania Daima jana kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, alisema tayari mteja wake(Mbatia) ameishalipa kiasi hicho cha fedha katika ofisi ya Mhasibu wa Mahakama na kwamba kiasi hicho cha fedha alikkiwasilisha yeye mahakamani kwaniaba ya mteja wake.

“Mahakama hii ilitupunguzia nafuu ya kiasi cha kulipa fedha kama dhamana ya kesi iliyofunguliwa na mteja wangu hapa mahakamani ambapo kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi, mlalamikaji anapaswa awe dhamana mahakamani ya shilingi milioni tano kwa kila mdaiwa hiyo mteja wangu asingeomba nafuu ya kunguziwa angepaswa kulipa jumla ya milioni 15 lakini kwakuwa aliomba apunguziwe mahakama hii ilimpunguzia kutoka kiwango hicho na kumtaka alipe jumla ya shilingi milioni kwa wadaiwa wote ambapo hapo sasa utaona kila mdaiwa anamuwekea dhamana ya shilingi milioni tatu badala ya milioni tano ya awali na kesi hiyo itakuja kwaajili ya kutajwa Mei 31 mwaka huu.”alisema Tibanyendera.

Mbali na Mdee wadaiwa wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo.Novemba 25 mwaka 2010 Mbatia alifungua kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo hilo ambayo yalimtangaza Halima Mdee(CHADEMA) kuwa ndiye aliyeshinda na ataliongoza jimbo hilo kwa kipindi cha miaka mitano.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Mei 19 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.