Header Ads

MELI YA TAWALIQ 1 HAIKUWA NA BENDERA-SHAHIDI

Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa 11 wa Upande wa Jamhuri katika kesi ya uvuvi haramu katika Bahari ya Hindi katika kina kirefu cha Ukanda wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayowakabili raia 36 wa kigeni maarufu kama ‘kesi ya samaki wa Magufuli’,Mrakibu Mwandamizi wa Polisi(SSP), Hussein Kashinde ameileza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, alikutaka mkoba mweusi kwenye chumba cha naodha wa Meli ya Tawariq 1, kilichokuwa na nyaraka za meli ya Tawariq 2.


SSP Kashinde ambaye alikuwa mpelelezi wa kesi hiyo na ndiyo alitoa hati ya ukaguzi wa meli hiyo, alitoa maelezo hayo wakati akiongozwa kutoa ushahidi wake na wakili mwandamizi wa serikali Biswalo Mganga,Prosper Mwangamila na kuhojiwa na wakili wa utetezi Ibrahim Bendera alidai kuwa wakati wanafanya ukaguzi walimshirikisha naodha wa meli hiyo na pia walipoikagua meli hiyo walibaini meli hiyo pia haikuwa na bendera inayoonyesha meli hiyo ya Tawariq 1 ilikuwa ikitokea nchi gain na kuelekea nchi ipi na kwamba hakuwa na nyaraka zozote zinazoonyesha meli hiyo ilikuwa imebeba mzigo gain.

“Baada ya kuipekua meli hiyo ya Tawariq 1 kwenye chumba cha naodha nilikuta mkoba mweusi wenye nyaraka za meli ya Tawariq 2 na nilipomhoji naodha alikiri kuwa nyaraka hizo ni zao na ni za meli nyingine ambazo zinamilikiwa na mtu mmoja na kwamba wanaruhusiwa kuzitumia katika meli ya Tawariq 1 ambayo imekamatwa ambaye hakumtaja kwa jina na pia tulibaini meli hiyo hakikuwa ikipeperusha bendera ya nchi iliyokuwa ikitoka na hilo ni kosa kisheria na pia hatukukuta nyaraka ambazo zingeonyesha meli hiyo ilikuwa imebeba mzigo gani na wenye uzito gani”alidai SSP-Kashinde.

Aidha alidai alipofika Bandari jijini Dar es Salaam, ambapo meli hiyo imetia nanga hapo kwaajili ya upekuzi alikadhibiwa jumla ya hati 32 za kusafiria wakati jumla ya washtakiwa hivi sasa ni 36 na kwamba wengi hawakuwa wamempatia hati zao za kusafiria kitendo ambacho alidai kuwa washtakiwa wengine ambao hawakuwa wamemkabidhi hati zao ina maana hawakuwa na hati hizo za kusafiria.

Hata hivyo wakili wa utetezi Ibrahim Bendera alimtaka shahidi huyo akisome kielelezo cha 22 ambacho ni hati ya upekuzi ambayo imesainiwa na shahidi huyo na nahodha ambapo Bendera aliiomba mahakama imruhusu mkarimani wa lugha ya Kichina kusoma kilichosainiwa na naodha huyo kwenye hati hiyo ambapo mkarimani huyo alisoma na kuieleza mahakama hiyo kuwa naodha huyo ambaye ni mshtakiwa wa kwanza aliweka saini yake na chini ya saini yake aliandika kuwa hafahamu lugha ya kiingereza hali iliyosababisha watu kuangua kicheko.

Wakili Bendera aliendelea kumuuliza shahidi huyo ni utarabu gani aliokuwa akiutumia kuwasiliana na mshtakiwa huyo ambapo shahidi huyo alidai kuwa alikuwa akitumia mtindo wa kumweleza nahodha ambaye ni raia wa china kupitia mkarimani wa lugha ya Kichina, Rahma Mohamed na kwamba hata alipomaliza kupekua alimpatia hati hiyo nahodha aisaini na kweli aliisani na kwamba mkarimani huyo Rahma Mohamed alimsomea shahidi huyo kuwa nahodha huyo alikuwa ameweka saini yake na kwamba hilo andishi la chini ya saini ya nahodha hiyo ambayo limetafsiriwa jana na mkarimani mwingine wa lugha ya kichina kuwa kilichoandikwa na naodha chini ya saini yake kuwa ‘hafahamu lugha ya kiingereza’ ni kigeni kwake.

Jaji Mwarija aliairisha usikilizaji wa kesi hiyo hadi leo ambapo shahidi wa 12 wa upande wa Jamhuri atapanda kizimbani kuanza kutoa ushahidi.Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mfululizo hadi Mei 31 mwaka huu.

Machi 9 mwaka 2009 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na makosa ya uvivu haramu katika kina kirefu cha habahari ya Hindi Ukanda ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuharibu mazingira ya ukanda huo.Hadi sasa washtakiwa wanaendelea kusota rumande kwa kukosa dhamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Mei 20 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.