Header Ads

LWAKATARE NJE KWA DHAMANA




Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana imempatia dhamana Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare na mwenzake Joseph Ludovick  wanaokabiliwa na kosa moja la kula njama utaka kumdhuru kwa sumu Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Denis Msacky.

Hakimu Mkazi wa Mahakama  Alocye Katemana alitoa uamuzi wa kumpatia dhamana Lwakatare na wenzake  jana saa mbili  asubuhi ambapo alisema jana kesi hiyo ilikuja kwaajili ya yeye kutolea uamuzi maombi ya dhamana na mapingamizi ya dhamana yaliyowasilishwa mahakamani hapo Mei 13 mwaka huu, na wakili wa washitakiwa hao Peter Kibatara na wakili wa jamhuri Prudence Rweyongeza na Ponsia Lukosi ambapo mawakili wa jamhuri waliomba mahakama isimpatie dhamana.

Hakimu Katemana alisema amefikia uamuzi wa kukubalina na mawakili wa washitakiwa walioomba mahakama iwapatie dhamana kwasababu ina mamlaka ya kufanya hivyo na kwamb anatupilia mbali ombi la mawakili wa upande wa jamhuri uliotaka mahakama isiwape dhamana kwasababu pingamizi hilo la upande wa jamhuri halina msingi wowote kisheria.

“Ili mshitakiwa apate dhamana ni lazima awe na wadhamini wawili wanaotoka taasisi zinazotambulika kisheria  ambapo kila kila mdhamini atatakiwa asaini bondi y ash.milioni 10 pamoja na washitakiwa wenyewe,washtakiwa hao kusamilisha hati zao za kusafiria mahakamani na kutotoka  nje ya jiji la Dar  es Salaam bila ya kuwa na kibali cha mahakama’alisema Hakimu Katemana.
 
Baada ya kumaliza kusoma masharti hayo ya dhamana, Hakimu Katemana  aliiahirisha kesi hiyo hadi nyakati za saa 8:00 mchana, kwa ajili ya kuwapa nafasi upande wa mashtaka ili kuweza kuhakiki barua zilizowasilishwa na wadhamini kama zilikuwa ni halali kisheria au la.
 
Wakati  upande wa mashtaka  ukienda kuhakiki barua hizo, washtakiwa hao walipelekwa rumande kwa ajili ya kusubiri  kusaini hati za dhamana  ili kuweza kuachiwa huru ama la.

Ilipofika saa nane mchana, washitakiwa hao waliingizwa kwenye chumba cha mahakama ambapo Hakimu Katemana aliaki nyaraka hizo za masharti ya dhamana na upande wa jamhuri ulikuwa hauna pingamizi, na akaamua kumpatia dhamana Lwakatare kwasababu alitimiza masharti hayo ya dhamana na alimyima dhamana Ludovick kwasababu alishindwa kutumiza masharti hayo na akaamuru Ludovick apelekwe rumande na kisha kuiarisha kesi hiyo hadi Juni 24 mwaka huu, kesi hiyo hadi Juni 24 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa.
 
Mei 13 mwaka huu, kesi ya msingi ya Lwakatare ilivyokuja katika Mahakama ya Kisutu kwaajili ya kutajwa, hakimu Alocye Katemana anayesikiliza kesi hiyo hakuwepo na mawakili wa Lwakatare Peter Kibatara aliwasilisha ombi la kuomba mteja wake apatiwe dhamana kwasababu kosa la kwanza la kula njama lilobaki linadhamana kwa mujibu wa sheria lakini hata hivyo wakili wa Serikali Prudence  Rweyongeza alililipinga ombi hilo kwa madai kuwa shauri hilo lipo hatua za uchunguzi  kilichopo mahakamani hapo ni jalada la tuhuma zinazowakabili washitakiwa ambazo zipo katika hatua za uchunguzi na kwamba tuhuma hizo mwisho wa siku zitakufunguliwa kesi rasmi Mahakama Kuu kwani Mahakama Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kuisikiliza hivyo huwezi mahakama haiwezi kutoa dhamana kwa kesi ambayo haipo(Pending Trial) .

“Na kwa mazingira ya shauri linalomkabili Lwakatare hapa Mahakama ya Kisutu,lipo katika hatua za uchunguzi na  bado DPP hajafungua kesi rasmi Mahakama Kuu, sasa tunashangaa mawakili wa washitakiwa wanawasilisha ombi la dhamana leo hii katika mahakama hii wakati maamuzi hayo ya mahakama ya Rufaa yapo na bado hajatenguliwa?

Rweyongeza aliomba mahakama hiyo itupilie mbali maombi ya mawakili wa utetezi kwasababu hakuna kesi rasmi iliyofunguliwa na DPP mahakama Kuu dhidi ya washitakiwa na kwamba shauri lililopo katika mahakama ya Kisutu lipo katika hatua za uchunguzi.

Mei 8 mwaka huu,Jaji Lawrence Kaduri wa Mahakama Kuu Kanda ya  Dar es Salaam, alitoa uamuzi wa kumfutia jumla ya  makosa matatu ya ugaidi baada ya kuona hati ya mshitaka haijitoshelezi kumfungulia mashitaka hayo na hivyo kumbakizia kosa hilo moja la kula njama na kuamuru kesi hiyo irudishwe katika mahakama ya Kisutu kwaajili ya hatua zaidi.

Mei 21 mwaka huu, Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi aliwasilisha ombi Mahakama ya Rufaa nchini, linaomba mahakama hiyo iitishe mwenendo wa uamuzi huo wa mahakama kuu ambao ulimfutia Lwakatare mashitaka hayo matatu na pia uutengue , na hadi sasa mahakama ya rufaa bado haijapanga tarehe wala majina ya majaji wa kaunza kusikiliza ombi hilo la DPP.

Machi 20 mwaka huu, Lwakatare na wenzake walifunguliwa rasmi kesi Na.6/2013  ya tuhuma za ugaidi ambapo kosa la pili, tatu, na la nne yalikuwa hayana dhamana na hivyo Mei 8 mwaka huu, Jaji Kaduri aliyafuta makosa hayo kwa maelezo kuwa hajaona kama kuna maelezo ya kutosha ya kuwafungulia mashitaka ya aina hiyo washitakiwa hao. 

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Juni 12 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.