Header Ads

MAHAKAMA YA RUFAA YATENGUA HUKUMU YAKE



Na Happiness Katabazi

HATIMAYE jopo la majaji watano wa  Mahakama ya Rufaa nchini limetungua hukumu iliyotolewa na jopo la majaji watatu wa mahakama mwaka 2011  ambayo ilikuwa ikimtaka mtu yoyote anayepinga ubunge wa mbunge aliyepo madarakani kuwasilisha kwanza mahakamani ombi la kuomba mahakama impangie kiwango cha kulipa dhamana ya kufungua kesi za uchaguzi ngazi ya ubunge.

Uamuzi huo wa ambao imeandika historia mpya katika tasnia ya sheria ya nchini, ulitolewa jana mchana na jopo la majaji watano wa Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam, Januaria Msofe, William Mandia, Salum Massati, Angela Kileo, Nataria Kimaro ambao walisema wamekubaliana na hoja za wakili wa kujitegemea Herbet Nyange ambaye  aliomba mahakama itoe tafsiri ya kifungu cha 111 cha Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010, kinachomtaka anayefungua kesi ya uchaguzi ya kupinga matokeo ya ubunge, kwanza alazimike kuwasilisha ombi mahakamani la kuomba mahakama impangie kiasi cha kulipa dhamana kabla ya kesi ya msingi kuanza kusikilizwa.

Jaji Msofe alisema jopo lake lilisikiliza hoja za wakili Nyange kuhusu kuomba tafsiri ya kifungu hicho na kuipitia hukumu iliyotolewa mwaka 2011 na jopo la majaji watatu wa mahakama hii, alisema wamekubaliana na hoja wakili Nyange ya kwamba ni kweli uamuzi wa rufaa ile ya jopo la majaji wa tatu ulikuwa na makosa.

“Kwa sababu hiyo jopo hili la majaji watano leo linatangaza kuwa limetengua uamuzi wa majaji wenzetu wa tatu ambayo ulikuwa unamtaka mtu yoyote anayewasilisha ombi la kupinga ubunge wa mbunge kuwasilisha kwanza ombi la kuomba pangiwe kiwango cha kulipa dhamana ya kuendesha kesi yake ya kupinga ubunge;

“Hivyo jopo letu linatamka kuwa kuanzia sasa mtu yoyote anayeta kufungua kesi ya kupinga ubunge hatalazimika tena kuanza kuwasilisha ombi mahakamani la kuomba apangiwe kiasi cha kulipa hivyo badala yake jopo hili linatoa ruhusa kwa mtu mwenye uwezo wa kifedha wa kulipa dhamana ya kufungua kesi ya kupinga kesi afungue kesi ya kupinga ushindi wa ubunge moja kwa moja na kwa yule mtu ambaye hana huwezo wa kifedha wa kuweka dhamana ya fedha mahakamani kama anavyoakiwa na sheria ya uchaguzi kulipa kwanza Sh.milioni tano, basi mtu huyo awasilishe ombi mahakamani la kuomba apunguziwe kiasi hicho cha fedha kwaajili ya dhamana ya kesi”alisema Jaji Msofe.

Aidha jaji huyo alisema baada ya mahakama yake kutoa uamuzi huo jana , mahakama yake imesema itaanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Chiriko dhidi ya Lugora katika tarehe ambayo itakuwa imepangwa na uongozi wa mahakama ya rufaa.

 Wakili Nyange ambaye anamtetea mwomba rufaa katika rufaa ya ubunge wa jimbo la  Mwibara, Chiriko Haruni Davidi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  dhidi ya Mbunge wa Mwibara Bunda, Mkoani Mara, Kangi Lugora, wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo Chiriko anapinga ubunge wa Lugora anatetewa na wakili   Melkizedeck Lutema  na Mwanasheria Mkuu wa Serikali anayetetewa na  wakili wa serikali Wakili wa Serikali Mkuu, Obadia Kameya akimwakilisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali  alioupata mwaka 2010 kuwa ushindi wake ulikuwa umekiuka sheria ya uchaguzi.
 Wakati Chiriko akikata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo katika rufaa  ya kesi ya uchaguzi iliyokuwa imefunguliwa na   Katani A. Katani (Chadema) dhidi ya Mbunge wa jimbo la (Tandahimba), Juma Njwayo ya mwaka 2011.  Naye Lugora  alikata rufaa mahakamani hapo  akipinga hukumu hiyo iliyompa ushindi.

Lugola katika rufaa yake , pamoja na mambo mengine, anadai kuwa mlalamikaji katika kesi ya msingi, Chiriko alilipa gharama za kufungua kesi hiyo bila kuiomba Mahakama impangie kiwango alichopaswa kutoa, kinyume cha kifungu hicho cha 111 cha Sheria ya Uchaguzi.
Wakili wa Lugora, Lutema akiongezea nguvu hoja yake alirejea  uamuzi wa Mahakama ya Rufani katika rufaa ya Katani A. Katani wa Chadema, dhidi ya Mbunge wa Tandahimba, Juma Njwayo ya mwaka 2011.

Ambapo kwa mujibu wa uamuzi wa jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo katika kesi hiyo iliyotolewa uamuzi wake mwaka 2011, walitupilia  mbali rufaa hiyo  ya  Katani kutokana na mlalamikaji kuwasilisha dhamana ya kesi bila kuomba mahakama impangie kiwango, kinyume cha kifungu hicho cha 111cha Sheria ya Uchaguzi.

Mei 17 mwaka huu, wakili wa Chiriko, Nyange, alidai kuwa uamuzi wa rufaa ya Katani haukuwa sahihi na kwamba mahakama haikutafsiri vizuri kifungu hicho.

Wakili Nyange  alidai kuwa uamuzi huo unakiuka marekebisho ya mwaka 2002 ya Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 1985, na kwamba unabadili msimamo wa mahakama hiyo ambao umekuwepo tangu mwaka 2006, bila kuubainisha msimamo huo wa mahakama hiyo.

Chanzo:Gazeti la Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Juni Mosi mwaka 2013.

1 comment:

Anonymous said...

At the same time brewer provides you with unique features attractive believe accomplish the
coffee enjoyment each time. The patient with good feeling sick, vomiting is as well
get injured through the process of coffee bean can also be happier drinking lemon juice and green tea.

All your little associates 're remarkably super understanding of sickly variations inside air flow for that reason even the tiniest differ through the temperatures ph amount will definitely extremely impact on that in the hazardous method as well as, it's wise that you don't placement whatever thing citrus to that were designed to simply turn citrus from the composting not unlike milk products, peelings range acid vegetables as with lemons so a melon. Should selected the many plunger and as a result screen method may be out of an media before you carry out. These types imagination might a fact before you style your espresso coffee by using the Gaggia Improvement Espresso Machine.

Here is my blog post: mr coffee 12 cup programmable coffeemaker

Powered by Blogger.