Header Ads

LWAKATARE KUPEWA,KUNYIMWA DHAMANA LEO?


Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,leo inatarajia kutoa uamuzi wa kumpa au kumnyima dhamana Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph wanaokabiliwa na kosa moja la kula njama kutaka kumuua kwa sumu Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Denis Msack.
Hayo yamesemwa jana na Hakimu Mkazi Alocye Katemana muda mfupi baada ya wakili mwandamizi wa serikali Ponsian Lukosi kuikumbusha mahakama kuwa kesi hiyo jana ilikuwa imekuja kwaaajili ya kutajwa.

Hakimu Katemana alisema anaiarisha kesi hiyo hadi leo ilikuja kuja kutoa uamuzi wa maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na mawakili wa Lwakatare, Peter Kibabatara na Abdalah Safari  Mei 13 mwaka mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo, wakati yeye alipokuwa likizo na mawakili wa upande wa jamhuri walipinga washitakiwa hao wasipewe dhamana.

Mei 13 mwaka huu, kesi ya msingi ya Lwakatare ilivyokuja katika Mahakama ya Kisutu kwaajili ya kutajwa, hakimu Alocye Katemana anayesikiliza kesi hiyo hakuwepo na mawakili wa Lwakatare Peter Kibatara aliwasilisha ombi la kuomba mteja wake apatiwe dhamana kwasababu kosa la kwanza la kula njama lilobaki linadhamana kwa mujibu wa sheria lakini hata hivyo wakili wa Serikali Prudence  Rweyongeza alililipinga ombi hilo kwa madai kuwa shauri hilo lipo hatua za uchunguzi  kilichopo mahakamani hapo ni jalada la tuhuma zinazowakabili washitakiwa ambazo zipo katika hatua za uchunguzi na kwamba tuhuma hizo mwisho wa siku zitakufunguliwa kesi rasmi Mahakama Kuu kwani Mahakama Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kuisikiliza hivyo huwezi mahakama haiwezi kutoa dhamana kwa kesi ambayo haipo(Pending Trial) .

“Na kwa mazingira ya shauri linalomkabili Lwakatare hapa Mahakama ya Kisutu,lipo katika hatua za uchunguzi na  bado DPP hajafungua kesi rasmi Mahakama Kuu, sasa tunashangaa mawakili wa washitakiwa wanawasilisha ombi la dhamana leo hii katika mahakama hii wakati maamuzi hayo ya mahakama ya Rufaa yapo na bado hajatenguliwa?

Rweyongeza aliomba mahakama hiyo itupilie mbali maombi ya mawakili wa utetezi kwasababu hakuna kesi rasmi iliyofunguliwa na DPP mahakama Kuu dhidi ya washitakiwa na kwamba shauri lililopo katika mahakama ya Kisutu lipo katika hatua za uchunguzi.

Machi 20 mwaka huu, Lwakatare na wenzake walifunguliwa rasmi kesi Na.6/2013  ya tuhuma za ugaidi ambapo kosa la pili, tatu, na la nne yalikuwa hayana dhamana na hivyo Mei 8 mwaka huu, Jaji Kaduri aliyafuta makosa hayo kwa maelezo kuwa hajaona kama kuna maelezo ya kutosha ya kuwafungulia mashitaka ya aina hiyo washitakiwa hao. 

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Juni 11 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.