Header Ads

WASHTAKIWA WASITISHA MGOMO WA KUTOFIKA MAHAKAMANI

Na Happiness Katabazi

WASHITAKIWA nane wa kesi ya uporaji wa sh mil. 150 katika benki ya Standard Chartered jijini Dar es Salaam, ambao wiki hii waliweka mgomo wa kutokwenda mahakamani wameamua kusitisha mgomo huo.

Mgomo huo umesitishwa juzi baada ya kufanyika kwa mazungumzo baina ya uongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu na watuhumiwa hao.

Kwa mujibu wa watuhumiwa hao, uongozi huo wa mahakama uliowatembelea gerezani, uliwahidi kuwa
kesi zao zitasikilizwa na katika kipindi cha miezi miwili zitakuwa zimemalizika.

Mei 7, mwaka huu, washtakiwa watano wa kesi nyingine ya uporaji wa zaidi ya sh milioni 233.8 uliofanyika katika duka la kubadilishia fedha za Kigeni la Maksons waligoma kula na kufika mahakamani kutokana na madai ya kutotendewa haki na mahakama.

Mahakama ya Kisutu imeshindwa kuwaleta mashahidi mahakamani tangu kesi hiyo ifunguliwe miaka mitano iliyopita.

Washtakiwa hao ni Martin Mndasha, Eric Mfinanga, Mashaka Mahengi, John Mndasha, Philip Mushi, Rashid Eliakim, Lucas Aloyce, na Jafar Mkenda.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Juni 10 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.