Header Ads

DECI HAIKUWA NA JUKUMU LA KUKUSANYA FEDHA-SHAHIDI

Na Happiness Katabazi
NAIBU Msajili wa Wakala wa Usajili wa Makampuni(BRELA), Neol Shani ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa kampuni ya Deci Tz Ltd haikuwa na jukumu la kukusanya amana kwa watu na kuwarudishia kwa riba.


Shani ambaye tisa wa upande wa Jamhuri katika kesi ya kuendesha na kusimamia mradi wa upatu na kupokea amana za umma bila leseni inayowakabili wakurugenzi wa kampuni ya DECI Tz Ltd , alitoa maelezo hayo wakati akiongozwa na wakili wa serikali Prospa Mwangamila mbele ya Hakimu Mkazi Stewart Sanga kutoa ushahidi wake ambapo alidai kuwa yeye ndiye aliyeshughulia fomu za kuomba kampuni hiyo isajiliwe isajiliwe na yeye ndiyo aliyeidhinisha isajiliwe kama kampuni baada ya waombaji ambao ni washtakiwa kukidhi vigezo.

Shahidi ambaye ni mwanasheria kitaaluma alieleza pia kuifahamu kampuni ya kigeni ya Deci Africa Ltd yenye makao makuu nchini Kenya kwasababu ilileta maombi BRELA ya kutaka kufungua tawi lake hapa nchini na maombi hayo ya kampuni ya kigeni aliyashughulikia yeye na kwamba yalikuwa yamekidhi vigezo vyote na akaisajili na kuongeza kuwa kwa mujibu wa maombi hayo yanaonyesha wawakili wa kampuni hiyo ya kigeni hapa nchini wakili wa kujitegemea Alex Mgongolwa na Jackson Mtales.

Akihojiwa na wakili wa washtakiwa Hudson Ndusyepo kwamba majukumu ya kampuni ya kigeni ya Deci Africa Ltd ni yapi ,na ofisi za makampuni hayo zipo maeneo gani hapa nchini , shahidi huyo akajibu kuwa hayakumbuki hali iliyosababisha wakili Ndusyepo kumhoji kuwa yeye ni mwanasheria na alikuwa anafahamu jana alikuwa anakuja mahakamani kutoa ushahidi na kwamba ndiyo yeye aliyeshughulikia usajili wa makampuni hayo inakuwaje anashindwa kufahamu majukumu ya kampuni hizo na ofisi zake jambo ambalo shahidi huyo aliendelea kusisitiza kuwa anashughulikia maombi mengi ya usajili wa makampuni hivyo siyo rahisi kukumbuka majukumu ya kila kampuni.

Mwaka 2009, washtakiwa katika kesi hiyo ni Jackson Mtares, Dominic Kisendi, Timotheo ole Loitgimnye, Samuel Mtares, Arbogast Kipilimba na Samuel Mtalis,walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza na Jamhuri ilidai kuwa washtakiwa wanamakosa ya kuendesha na kusimamia mradi wa upatu kinyume na sheria pamoja na kupokea amana za umma bila leseni na Na upande wa Jamhuri unawakiliwa na Mwanasheria wa Kanda ya Dar es Salaam, Justus Mulokozi na Prosper Mwangamila.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa Aprili 29 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.