Header Ads

SHAHIDI SERIKALI ILIIBEBA RICHMOND

Na Happiness Katabazi

MTAALAMU wa manunuzi wa Shirika la Umeme (TANESCO), Nicholaus Suke ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kuwa Kamati maalumu iliyoundwa na Shirika hilo kuchambua washiriki walijitokeza katika zabuni ya kununua mashine ya kufua umeme wa megawati 100 ilibaini hakuna aliyekidhi vigezo vilivyowekwa ikiwemo kampuni ya Richmond Development Company LLC.


Suke mbaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema alitoa maelezo hayonjana wakati akiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali Fredrick Manyanda kutoa ushahidi wake katika kesi ya kutoa taarifa za uongo kwa maofisa wa serikali kuhusu kampuni ya Richmond inayomkabili Naeem Gire ambapo shahidi huyo alidai kuwa licha ya kamati hiyo kuchambua makampuni yale , lakini ilibaini hakukuwa na kampuni yenye uhafadhari.

Alidai kuwa mwaka 2005 alikuwa na wadhifa wa Afisa na Katibu wa Bodi ya Zabuni na kwamba anaitambua kampuni hiyo ambayo mwaka 2006 ilikuwa ni miongoni mwa makampuni nane yaliyojitokeza kuomba zabuni hiyo iliyotangazwa na serikali kutoka na taifa kukumwa na tatizo la umeme.

Alitaja baadhi ya washiriki waliowasilisha makabrasha ya maombi ya kupatiwa tenda ya zabuni hiyo ambayo ilitangazwa kwenye magazeti, mbali ya Richmond ni Aggreco, Real Energy, Gapco, Apgum, Quatus, Recno.

Shahidi huyo alidai zabuni hiyo ilikuwa ya wazi ya ushindani wa kimatafa ambapo ilitangazwa Februari mwaka 2006, baada ya Bodi ya manunuzi ya serikali kupitisha nyaraka za kuanzisha mchakato wa kuitangaza.Hata hivyo, zabuni hiyo ilitangazwa kwa siku 10, kinyume na sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 inayotaka iwe ya siku 45 na ilifanyika hivyo kutokana na maelekezo ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Dk. Ibrahim Msabaha ambaye baadaye alikuja kujiudhulu kutokana na kashfa ya mkataba huo wa Richmond.

Alidai siku ya ufunguzi wa zabuni hiyo, kulikuwa na marumbano baina ya TANESCO na serikali. Alidai Richmond ilifuata taratibu zote za kushiriki kwenye zabuni. Baada ya washiriki hao kuwasilisha makabrasha yao, kamati maalumu iliundwa kuchambua washiriki hao ikiwa chini ya mwenyekiti Boniface Njombe akisaidiwa na washauri kutoka kampuni ya Lamahye kutoka Ujerumani ambao ni Poule na Hunae.

Shahidi huyo alieleza kuwa matokeo matokeo ya uchambuzi yaliweka wazi kwamba hakuna mshindi katika zabuni hiyo kwasababu hakuna hata kampuni moja kati ya zote zilizoomba zilitimiza vigezo vilivyowewa.Alidai bodi ya zabuni ilipopelekewa taarifa na kamati hiyo, iliridhia matokeo hayo, na kwa sababu nchi ilikuwa na matatizo ya umeme Bodi ya TANESCO kupitia menejimenti ilijulishwa kuhusu hilo ambapo iliiagiza kamati hiyo kuangalia kama kuna kampuni yenye uhafadhali.

Shahidi huyo, alidai kamati hiyo ilifanya uchambuzi tena ambapo ilibaini hakuna mwenye hafadhali na serikali ilijulishwa kwa kupitia bodi ya TANESCO. Alidai serikali ilielekeza kupelekewa kwa nyaraka za zabuni ambapo ili ziende bodi ya TANESCO ilifuta zabuni na kuzipeleka nyaraka.Mtaalamu huyo, alidai serikali ilitengeneza kamati yake maalumu na kuendelea na mchakato huo, ambapo yeye hakuwepo.

Yafutayo ni mahojiano baina ya shahidi huyo na wakili wa mshtakiwa Alex Mgongolwa:
Mgongolwa: Ulisema kulikuwa na malumbano kati ya TANESCO na serikali ni malumbano gani?

Shahidi: Yalikuwa ni ya aidha zabuni itangazwe ya siku 10 au ifiatwe sheria ya manunuzi inavyosema. Malumbano hayo ilikuwa ni kuhakikisha sheria uinafuatwa.

Alidai TANESCO baada ya kuona sheria inavunjwa walitaarifu Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), ambayo ilishauri kufuatwa kwa njia nyingine ya kutangazwa kwa siku 14.

Shahidi huyo, alidai wao waliitaarifu serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini na kusisitiza agizo lao na siku 10 litekelezwe.

Shahidi wa pili kwenye kesi hiyo, alikuwa Wakili wa kujitegemea Silvester Shayo, ambaye alidai Machi 13, 2006 alikuwa shuhuda wa waraka wa kuteua mwakilishi baina ya kampuni ya Richmond na Gire ambaye aliteuliwa kuwa mwakilishi wa kampuni hiyo.

Alidai waraka huo aliletewa ofisini kwake na karani wa wakili mwenzake Emmanuel Kisusi na kwamba haukutilia shaka kwa kuwa anamuamini wakili huyo.Hakimu Lema aliairisha kesi hiyo hadi leo ambapo shahidi wa tatu atapanda kizimbani kuanza kutoa ushahidi wake.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Aprili 12 mwaka 2011.



No comments:

Powered by Blogger.