Header Ads

DPP AKWAMISHA KESI YA KAJALA

Na Happiness Katabazi

UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya kutakatisha fedha haramu inayomkabili Msanii wa Filamu nchini, Kajala Masanja na mumewe Faraja Chambo jana ulishindwa kuleta hati ya mashtaka iliyofanyiwa marekebisho kama ulivyoamliwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wiki iliyopita kwa madai kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP),Dk.Eliezer Feleshi juzi hakuweza kupatika ofini kwake ili aweze kutoa kibali cha kuletwa kwa hati hiyo mahakamani hapo.


Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mussa Hussein aliikumbusha mahakama hiyo kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya upande wa jamhuri kuleta hati ya mashtaka iliyofanyiwa marekebisho lakini ameshindwa kufanya hivyo kwasababu juzi DDP-Dk.Feleshi hakuwepo ofisini kwake ili aweze kutoa kibali cha kuletwa hati hiyo mahakamani na kwasababu hiyo wanaomba wapewe siku moja waweze kuileta hati hiyo mahakamani.

Kwa upande wake Hakimu Mkazi Sundi Fimbo alikataa hati hiyo isiletwe leo na badala yake hati hiyo iletwe Machi 26 mwaka huu kwaajili wa washtakiwa kusomewa upya mashtaka hayo na akaamuru mshtakiwa arudishwe rumande , uamuzi ambao ulikubaliwa na wakili huyo wa Takukuru na wakili wa Kajala, Alex Mgongolwa.

Machi 15 mwaka huu, Kajala na mumewe ambaye hata hivyo mumewe yupo gerezani anakabiliwa na kosa la utakatishaji fedha haramu katika kesi nyingine ambapo kwa mujibu wa sheria kosa hilo halina dhamana.Wakili wa Takukury, alidai washtakiwa hao wanakabiliwa na matatu, kosa la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 ambapo washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo la kula njama la kuamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam.

Shtaka la pili ni ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007. Na shtaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda siku hiyo ya Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijiua ni kinyume na sheria hiyo.

Hata hivyo baada wakili huyo wa Takukuru siku hiyo kumsomea mashtaka hayo, Wakili Mgongolwa alidai hati hiyo ya mashtaka ina mapungufu ya kisheria kwasababu hati hiyo ya mashhata haijasema nyumba hiyo iliuzwa kwa nani na kwamba nyumba hiyo ipo katika Kitaly gani, hoja ambayo ilikubaliwa na Hakimu Fimbo Machi 20 mwaka huu, ambapo aliuamuru upande wa Jamhuri ukaifanyie marekebisho hati hiyo na kisha jana uje na hati ya mashtaka ambayo imeishafanyiwa marekebisho.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Machi 23 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.