Header Ads

KESI YA NG'UMBI,MNYIKA KUANZA KUUNGURUMA LEO



Na Happiness Katabazi

ALIYEKUWA mgombea Ubunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), Hawa Ng’umbi leo anatarajia kupanda kizimbani katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kutoa ushahidi wake katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa jimbo hilo wa mwaka 2010 ambayo yalimtangaza John Mnyika(CHADEMA) kuwa mshindi.


Ng’umbi ambaye amewahi kuwa mkuu wawilaya ya Mvomero, Makete na Bukombe ambaye anatetewa na wakili wa kujitegemea Issa Maige ataanza kujitetea mbele ya Jaji Upendo Msuya ambapo kesi hii in aanza kusikilizwa mfululizo kuanzia leo.

Novemba mwaka 2010, Ng’umbi alimfungulia kesi hiyo Na.107/2010 Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mnyika na Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo, akiiomba mahakama hiyo itangaze kuwa matokeo yaliyompa ushindi Mnyika ni batili kwasababu yalikiuka taratibu za Sheria ya Uchaguzi na kanuni zake ya mwaka 2010 na kwamba mdaiwa wa kwanza na wa tatu walishindwa kutimiza wajibu wao kikamilifu.

Kwa upande wake Mnyika ambaye anatetewa na wakili Edson Mbogoro alipinga madai hayo na kwamba taratibu za uchaguzi hazikukiukwa wakati wa zoezi zima la kuhesabu kura hadi Tume ya uchaguzi ilipomtangaza yeye kuwa ndiye mbunge wa jimbo hilo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatatu, Machi 19 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.