Header Ads

KAJALA ASOMEWA MASHTAKA UPYA

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE upande wa Jamhuri katika kesi ya kutakatisha fedha haramu inayomkabili msanii wa Filamu nchini Kajala Masanja na mumewe Faraja Chambo jana uliwasilisha hati mpya ya mashtaka waliyoifanyia marekebisho na kisha kuwasomea upya washtakiwa yanayowakabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.


Hatua hiyo ya kuwasilisha hati hiyo iliyofanyiwa marekebisho inatokana na amri iliyotolewa na Hakimu Mkazi Sundi Fimbo , Machi 15 mwaka huu, muda mfupi baada wakili huyo wa mashtaka kuwasomea mashtaka washtakiwa hao kwa mara ya kwanza na wakili wa utetezi Alex Mgongolwa kuomba mahakama hiyo iuamuru upande wa Jamhuri upanyie marekebisho hati hiyo kwasababu hati hiyo haijataja jina la mtu aliyeuziwa nyumba na washtakiwa hao na kwamba haikutaja nyumba hiyo iliyouziwa ipo katika Kitalu namba ngapi, ombi ambalo lilikubaliwa na hakimu huyo.

Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) Leonard Swai jana akiwasomea upya mashtaka ambayo imeletwa mahakamani hapo kwa kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Dk.Eliezer Feleshi, licha ya mume wa kaja kutokuwepo mahakamani kwasababu yupo gerezani akikabiliwa na kesi nyingine ya utakatishaji fedha ambayo haina dhamana kwa mujibu wa sheria, alidai kuwa washtakiwa hao wanakabiliwa na mashataka yale yale ya awali ambayo ni matatu na kwamba jina la mtu aliyeuziwa nyumba hiyo na washtakiwa hao ni Emilian Rugalia na kwamba nyumba hiyo iliyopo

Wakili wa Takukuru, alidai washtakiwa hao wanakabiliwa na matatu, kosa la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 ambapo washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo la kula njama la kuamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala eneo ambalo halijapimwa jijini Dar es Salaam.

Shtaka la pili ni ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo ambayo walikuwa wakiimiliki kwenda kwa Emilian Rugalia ambaye ndiyo walimuuzia kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya TAKUKURU ya mwaka 2007. Na shtaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda siku hiyo ya Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijiua ni kinyume na sheria hiyo.

Hata hivyo Kajala ambaye alikuwepo peke yake mahakamani hapo bila mshtakiwa wa kwanza (Chambo) ambaye ni mumewe kutokuwepo mahakamani hapo kwasababu yupo gerezani kwa zaidi ya mwaka mmoja kwasababu anakabiliwa na kesi nyingine ya utakatishaji fedha haramu iliyofunguliwa mahakamani hapo ambapo kwa mujibu wa sheria kosa hilo halina dhamana, alikana mashtaka yote matatu na akaamuriwa kurudishwa rumandwa hadi Aprili 4 mwaka huu, kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Machi 28 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.