Header Ads

MAWAKILI WA UTETEZI WAKWAMISHA YA RICHMOND

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana ilijikuta ikishindwa kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) dhidi ya aliyekuwa kigogo wa Kampuni ya Kufua umeme ya Richmond LLC , Naeem Gile kupinga uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwaka jana ulimuona mshtakiwa huyo hana kesi ya kujibu.


Rufaa hiyo Na.126 ya mwaka jana , ambayo inasikilizwa na Jaji Lawrence Kaduli jana ilikuja kwaajili ya kuanza kusikiliza sababu za mrufani(DPP), ambaye anawakilishwa na Mawakili Wakuu wa Serikali Stanslaus Boniface na Fredrick Manyanda ambapo jaji huyo alisema anakubaliana na sababu za mawakili wa utetezi zilizoomba rufaa hiyo isisikilizwe jana na hivyo akaiarisha kesi hiyo hadi Aprili 18 itakapokuja kusikilizwa.

Awali Mawakili wa Gile, Alex Mgongolwa jana aliomba mahakama iairishe usikilizwaji wa rufaa hiyo kwasababu juzi ndiyo mshtakiwa huyo ameingia nae mkataba wa kuanza kumtetea katika rufaa hiyo kwani kipindi kile mshtakiwa anashtakiwa katika Mahakama ya Kisutu alikuwa akimtetea na mkataba wao ulimalizika pale mahakama ile ya chini ilipotoa uamuzi wa kumuona ana kesi ya kijibu hivyo anaomba apewe muda akapitie hoja za mawakili wa serikali katika rufaa hiyo.

Aidha Mgongolwa alieleza sababu nyingine ya kuomba usikilizwaji wa rufaa hiyo uairishwe ni kwamba wakili wa Gile, Richard Rweyongeza yupo katika kesi kusafirisha kilo 92.2 za dawa ya kulevya aina ya Heroine yenye thamani ya sh bilioni mbili inayomkabili Assad Azizi Abdulasul ambaye ni mdogo wake aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ambayo imeanza kusikilizwa mfululizo kuanzia Jumatatu ya wikik hii na Jaji Kipenka Mussa katika Mahakama Kuu Kanda ya Tanga.

Katika rufaa hiyo DPP anaomba Mahakama Kuu itengue uamuzi wa mahakama hiyo ya chini iliomuona Gile hana kesi ya kuiibu kwasababu mahakama hiyo ilikosea kisheria kutoa uamuzi huo.

Julai 27 mwaka 2011 , Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Waliarwande Lema alitoa uamuzi wa kumuona Gile aliyekuwa akikabiliwa na makosa ya kughushi, kutoa taarifa za uongo kwa maofisa wa serikali kuhusu kampuni ya Richmond LLC ya Texas ya Marekani kuwa hana kesi ya kujibu kwasababu ushahidi ulitolewa na upande wa Jamhuri ni dhahifu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima na Alhamsi, Machi Mosi mwaka 2012

No comments:

Powered by Blogger.