Header Ads

MTEJA AIBURUZA AIRTEL KORTINI

Na Happiness Katabazi

MTEJA wa kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel Tanzania,Bernard Samson Thobias ameifungulia kesi ya madai ya ya fidia ya shilingi milioni 60 kampuni hiyo katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam, akitaka imlipe kiasi hicho cha fedha kwasababu ilimtangaza yeye kuwa ndiye mshindi wa Promosheni ya Kwanjuka sms Promotion lakini ikashindwa kumlipa shilingi 50,000,000 alizoshinda.

Thobias ambaye ni mlemavu wa masikio asiyesikia vizuri na anatetewa na wakili wa Kituo cha kutetea Haki za Binadamu, Fulgence Masawe amefungua kesi hiyo ya madai namba 12/2012 ambayo tayari imeishapangwa kwa Hakimu Rusema kwaajili ya kusikiliza.

Kwa mujibu wa hati ya madai ambayo gazeti hili inalo, inaeleza kuwa Thobias ni mteja wa kampuni ya airtel na ni mmiliki aliyeandikishwa na namba yake ni 0686-163144. Na bahati nasibu hiyo ilianza kuchezeshwa na kampuni hiyo kuanzia Aprili hadi mwanzo mwa Agosti 2011.Na kwamba Thobias alianza kushiriki kwenye bahati nasibu hiyo Mei ,2011 na mshindi alikuwa akitakiwa apewe Shlingi milioni 50.

Wakili Masawe anadai kuwa mteja wake huyo alianza kushiriki mchezo huo kuanzia Agosti 2011 na akajikusanyia zaidi ya pointi milioni 20 katika mchezo huo ambao mshindi alitakiwa apewe shilingi milioni 50, na kwamba Agosti 4 mwaka jana, na tangazo la yeye kuwa ndiye ameibuka mshindi lilitangazwa na mfanyakazi wa kampuni hiyo ambae alikuwa akitumia namba 0784 100778.

Wakili huyo anadai, baada ya mdaiwa kumpigia simu hiyo mteja wake, mteja wake aliamua kutoa kijijini alikokuwa akiishi na kuja katika ofisi za airtel kwaajili ya kufuatilia hiyo zawadi yake lakini alipofika katika ofisi za mdaiwa na kujitambulisha aliaelezwa na ofisa mmoja wa kampuni hiyo yeye siyo mshindi ila ameshindwa shilingi milioni moja za kitanzania na kwamba kwa ajabau hata hiyo shilingi milioni moja aliyoelezwa ameshinda hakupewa na kampuni hiyo hadi sasa.

“Mteja wangu kupitia wakili wake kabla ya kufungua kesi hii tulifanya juhudi za kuwasiliana uongozi wa juu wa kampuni hiyo kujua ni kwanini wanakataa kumlipan fedha hiyo aliyoshijnda, mdaiwa katika majibu yake alikiri kampuni yake kumpigia simu ya kumualifu kuwa ameshinda lakini kampuni hiyo ilishangaa wakati lipompigia simu mwanzo alipokela mlalamikaji lakini baada ya muda simu hiyo ikapokelewa na mkewe….na kwamba Thobias ni mlemavu wa masikio na asikii vizuri na kwamba uthibitisho wa kuwa yeye ni mgonjwa wa masikio umeandikwa katika ripoti ya uchunguzi uliofanywa na madaktari wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili’alidai wakili Masawe.

Aidha alidai kuwa kwa sababu kampuni hiyo ndiyo iliyompigia simu mteja wake kuwa ameshinda na anastahili kupokea zawadi hiyo hajapewa eti kwasababu simu aliyopigiwa ilipokelewa na mkewe na hivyo kampuni hiyo kuchanganyikiwa na kwakuwa mteja wake amekuwa mara kwa mara akifika katika ofisi za kampuni hiyo kudai zawadi yake bila mafanikio, anaiomba mahakama iiamuru kampuni hiyo imlipe sh milioni 60 kama fidia ya usumbufu alioupata.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Machi 13 mwaka 2012

No comments:

Powered by Blogger.