Header Ads

KAJALA KUSOTA RUMANDE


Na Happiness Katabazi

MSANII wa Filamu nchini, Kajala Masanja na mumewe Faraja Chambo jana walijikuta wakiifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabili na makosa matatu likiwemo kosa la kutakatisha fedha haramu.


Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKUKURU), Leonard Swai mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo alidai kuwa washtakiwa hao ambao ni wanandoa na wanatetewa na wakili wa kujitegemea Alex Mgongolwa wanakabiliwa na makosa matatu.

Wakili Swai alidai kuwa kosa la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 ambapo washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo la kula njama la kuamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam.

Shtaka la pili ni ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007.

Alidai shtaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda siku hiyo ya Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijiua ni kinyume na sheria hiyo.

Hata hivyo mshtakiwa wa pili (Chambo) wakati wanasomewa mashtajka hayo jana hakuwepo mahakamani kwasababu yupo gerezani kwakuwa anakabiliwa kesi nyingine ya utakatishaji fedha ambayo ipo katika mahakama hiyo na kwa mujibu wa sheria kosa la kutakatisha fedha halina dhamana.

Kajula alikanusha mashtaka hayo na wakili Swai alidai upelelezi bado haujakamilika.Hakimu Fimbo aliarisha kesi hiyo Aprili 20 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na akaamuru Kajala arudishwe rumande kwa sababu kosa la kutakatisha fedha linamkabili halina dhamana kwa mujibu wa sheria.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Machi 16 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.