Header Ads

MTIKILA AMKATAA HAKIMU FIMBO

Na Happiness Katabazi

IKIWA ni siku chache baada ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Sundi Findo, atoe uamuzi wa kumuona Mwenyekiti wa chama cha Democratic(DP), Mchungaji Christopher Mtikila ana kesi ya kujibu katika kesi ya kuchapisha na kusamba waraka wa uchochezi dhidi ya Rais Jakaya Kikwete , Mtikila amewasilisha mahakamani hapo ombi la kumuomba hakimu huyo ajitoe kwenye kesi yake ya jinai Na.132/2011 kwasababu hawezi kumtendea haki.


Kwa mujibu wa barua hiyo ambayo Tanzania Daima inayo nakala yake,Mtikila anamuonmba hakimu Fimbo ajitoe kwenye kesi yake kwasababu amebaini hawezi kumtendea haki kwasababu wakati kesi hiyo ikiendelea Mtikila ambaye ni mshtakiwa katika kesi hiyo aliwasilisha ombi la kuomba usikilizwaji wa kesi hiyo usimame hadi kesi ya Kikatiba iliyopo mbele ya Jopo la Majaji wa tatu wa mahakama Kuu wanaongozwa na Jaji Fakhi Jundu na Profesa Ibrahim Juma ambapo katika kesi hiyo anaiomba mahakama hiyo izifute sheria za makosa ya uchochezi kwakuwa zinanyima haki wananachi ya kutoa maoni yao itakapotolewa uamuzi lakini huyo alilikataa ombi lake.

Mtikila alidai kuna kesi tatu za Kikatiba zilizokuwa zimefunguliwa mahakama kuu na washtakiwa wanaokabiliwa na kesi za jinai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambao ni Jayantkumar Patel ‘Jeetu Patel’, Profesa Costa Mahalu na mahakama ya Kisutu ilisitisha usikilizwaji wa kesi zinazowakabili hadio mahakama kuu ilipozitolea uamuzi kesi zao za Kikatiba.

“Na huyu Hakimu Fimbo anafahamu fika nimefungua kesi ya Kikatiba Mahakama Kuu kuzipinga sheria za uchochezi ambao sheria hizo ndizo zimetumika kunifungulia kesi ya uchochezi iliyopo mbele yake na anafahamu fika kesi ya aina hiyo ikishafunguliwa mahakama ya juu, mahakama ya chini inatakiwa isitishe usikilizaji wa yangu hadi mahakama hiyo ya juu itakapotoa uamuzi lakini yeye amekuwa akilikataa ombi langu na kwa kitendo chake hicho minasema amevunja mwenendo wa kesi na ukiukwajili wa maadili ya sheria za nchi na haki na nimuomba ajitoe kwenye kesi yangu kwani tayari ameishaonyesha hawezi kunitendea haki ”alidai Mtikila.

Aidha Mtikila alidai sababu nyingine ya kumkataa hakimu Fimbo, ni kwamba wakati kesi hiyo ikiendeshwa aliwai kuwasilisha ombi la kutaka afutiwe kesi hiyo ya uchochezi kwasababu kesi hiyo ilifunguliwa nje ya muda kwani kesi za uchochezi zinatakiwa zifunguliwe mahakamani ndani ya miezi sita tangu mshtakiwa alituhumiwa kutenda kosa hilo na kwamba kesi hiyo inafanana na kesi ya madai ya fidia Na.166/2004 inayosikilizwa na Jaji Robert Makaramba , ambapo katika kesi hiyo anamdai Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa alikamatwa kinyume na sheria na kwamba kesi ile ambayo nayo ni ya uchochezi iliyokuwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni ilifunguliwa nje ya muda.

“Na maoni ya wananchi wengi baada ya uamuzi wako wa kuniona mimi nina kesi ya kujibu wananchi wengi wameuchukulia uamuzi huo ni wa kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete ambaye ni mpinzani wangu kidini na kisiasa na kwamba kitendo hicho kitavuruga uhuru wa mahakama na utu wangu”alidai Mtikila.

Alipotafutwa na waandishi wa habari kuthibitisha kama mahakama imepokea barua hiyo, Kaimu Hakimu Mkuu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Frank Moshi alikiri mahakama hiyo kupokea barua hiyo na kwamba taratibu nyingine za kiutawala zitafanyika baada ya Hakimu Mkuu Mfawidhi Elvin Mugeta akirejea ofisini kwani hivi sasa yupo nje ya Dar es Salaam, kwashughuli za kikazi.

Machi 13 mwaka huu, Hakimu Fimbo alimuona Mtikila ana kesi ya kujibu katika kesi ya uchochezi ambapo Hakimu Fimbo alisema baada ya kupitia ushahidi wa upande wa Jamhuri,amefikia uamuzi wa kumuona Mtikila ana kesi ya kujibu na kwamba maana hiyo Mtikila atatakiwa na mahakaa hiyo kupanda kizimbani Aprili 11 mwaka huu kwaajili ya kuanza kujitetea. Na Mtikila siku hiyo akaeleza kuwa amekusudia kuleta mashahidi 10.

Ilidaiwa kuwa kati ya Januari mwaka 2009 na Aprili 17, mwaka 2010 jijini Dar es Salaam, kwa nia ya uchochezi mshitakiwa alisambaza kwa umma nyaraka zilizosema 'Kikwete kuuangamiza ukristo', 'wakristo waungane kuweka mtu Ikulu' alinukuliwa Mtikila.

Katika shitaka la pili, Aprili 16, mwaka 2010 eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam, bila kibali alikutwa akimiliki waraka wenye uchochezi kwa jamii.Na katika kesi hii Mtikila hana wakili wa kumtetea na anajitetea mwenyewe.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Machi 23 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.