Header Ads

MAHAKAMA YA KISUTU YAKAGUA KANISA LA KKKT MBAGALA LILOALIBIWA NA BAADHI YA WAISLAMU

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilitembelea Kanisa la Kiinjili la Kilutheri  Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Jimbo la Kusini  Usharika wa Mbagala  ambalo washtakiwa 10 ambao ni waumini wa dini ya Kiislamu wanatuhumiwa kulifanyia uharibifu huo  ambapo lililikagua kanisa hilo na ikatoa  amri ya kuliruhusu kanisa lianze kufanya ukarabati wake .
 
Hakimu Mkazi Waliarwande Lema ambaye anaisikiliza kesi hiyo ya unyanganyi wa kutumia silaha ndiye aliyeongoza msafara wa washtakiwa 10, maofisa  wa Jeshi la Magereza , Polisi na wanahabari kutembelea eneo hilo ambapo msafara ulianzia mahakama ya Kisutu kwenda katika eneo la kanisa hilo na kujionea uharibu huo.
 
Hakimu Lema   ambaye alikuwa akipewa maelezo  ya uharibifu huo na  Mhasibu wa kanisa hilo, Bernad Maimu na Wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka na wakili wa washtakiwa ambapo waliiingia hadi ndani ya kanisa hilo na kulizunguka kanisa hilo, alisema mahakama imeishaona uharibifu huo na inatoa amri ya kuutaka uongozi wa kanisa uendelee na ukarabati wao na akaiarisha kesi hiyo hadi Januari 21 mwaka huu, itakapokuja kwaaji ya mashahidi wa upande wa jamhuri kuanza kutoa ushahidi wao na akaamuru washtakiwa hao warejeshwe rumande kwa sababu kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha linalowakabili halina dhamana.
 
Wakati Hakimu Lema akikagua kanisa hilo na msafara aliokuwa ameongozana nao usiopungua watu zaidi ya 40 , baadhi ya wakazi wa eneo la  Mbagala Zakhiem Kata ya Chalambe  ambapo ndipo lililopo kanisa hilo,walikuwa ni watu wenye utulivu na usalama uliimalishwa na wakazi hao walikaa mbali ya eneo  hilo la Kanisa ambapo mahakama jana iliamia hapo.
  
Awali jana asubuhi kabla ya mahakama kuamia eneo la tukio, Wakili Kweka aliileza mahakama kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya upande wa jamhuri kuwasomea washtakiwa hao ambao ni Hamad Sengondo,  Shogo Mussa,  Mashaka Iman, Hamza Mohamed, Mikidadi Sadiki, Juma  Jumanne, Issa Suleiman, Hamis Masoud Ramadhan Mohamed na Mohamed  Yusuf kusomewa maelezo ya awali.
 
Wakili Kweka akiwasomea maelezo ya awali alieleza kuwa  Oktoba 12 mwaka jana, vijana wadogo wenye umri wa chini ya miaka 18 walikuwa wanacheza  pamoja na kubadilishana mawazo, mmoja wa vijana hao alikojolea kitabu kitakatifu cha Waumini wa dini ya Kiislamu (Quran).
 
“Tukio hilo liliripotiwa  kwa wakubwa hao na Kituo cha Polisi Mbagala na wakati hatua zaidi zinataka kuchukuliwa  ndipo kundi la vijana  walijhitokeza  na kuafaamia ofisi za taasisi za serikali na nyumba za ibada za dini ya Kikristo”alidai Kweka.
 
Aidha alidai kuwa washtakiwa hao walikuwa ni miongoni mwa kundi lile lilofanya uharibifu huo katika kanisa hilo la KKKT Mbagala  na wakati wakitekeleza uhalifu huo   walikuwa wamebeba silaha ambazo ni nondo na matofali na kuvunja ukuta wa kanisa hilo na kisha kuvunja milango iliyokuwa imetengenezwa kwa madini ya Alminiam, meza, mabenchi, viti vya plastiki, madhabahu,  mfumo wa umeme, ,sofa seti, , makamati na  na grii.
 
“Na kama hiyo haitoshi  walichoma Altale na ofisi ya SACCO  ya kanisa hilo la ofisi ambayo ilikuwa ikitumiwa na mchungaji wa kanisa hilo, kuvunja kwa mawe maeneo mbalimbali ya kanisa hilo ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa vioo ambapo vitu vyote hivyo vina thamani ya Sh milioni 500.
 
“Vile vile  washtakiwa hao  waliiba Laptop, kinanda  cha umeme, spika , saa za ukutani ambapo vitu vyotye hivyo vina thamani ya Sh milioni 20. Na katika  kuakikisha  watamiza uhalifu huo walimtishia kwa silaha mlinzi wa kanisa za matofali na nondo Michael Samwel…..na tukio hilo lililipotiwa polisi na washtakiwa wote wakakamatwa  wakafikishwa mahakamani hapo hadi leo tunawasomea maelezo ya awali”alidai Kweka.
 
Hata hivyo washtakiwa hao walikana mashtaka yao na maelezo hayo na kwamba wao siyo waliotenda makosa hayo ila wanakubali makabila,kazi na majina yao.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Januari 7 mwaka 2013  

No comments:

Powered by Blogger.