Header Ads

MSHTAKIWA-NAJUA SIRI NYINGI ZA MWINYI


Na Happiness Katabazi

MTUHUMIWA anayedaiwa kumuibia  rais mstaafu All Hassan Mwinyi sh.milioni 37,440,000 , Abdallah Nassor Mzombe(40)  zikiwa ni kodi ya pango  katika nyumba  mbili zinazomilikiwa na rais huyo mstaafu, jana ameomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imentedee haki kwani hakunda makosa hayo.

Mzombe aliyatoa maombi hayo jana mbele ya Hakimu mkazi Jenevitus Dudu wakati alipopanda kizimbani kutoa utetezi wake, alidai kuwa kwanza alikuwa akifanya shughuli nyingi za wazi na za siri za rais Mwinyi  ambazo hata watoto wake wa kuwazaa hawazijui na kwamba anashangazwa kuona leo hii anashtakiwa kwa makosa ya kumuibia kiasi hicho cha fedha rais huyo Mstaaafu.

“Mheshimiwa hakimu mimi sina crown,sina fedha na hao wapangaji waliokuja kutoa ushahidi kuwa walinipa kodi mimi sikumpelekea Mwinyi ni waongo na sijawahi kugombana nao isipokuwa mpangaji mmoja tu ambaye tangu mwanzo nilimuona kama nimkorofi…..na kwakuwa Mwinyi ni kiongozi mkubwa ni wazi mashahidi hao wanaweza wakawa walishinikizwa kuja kutoa ushahidi wa kuja kunikandamiza mimi kwasababu wakipewa maelekezo ya kuja kufanya hivyo hawawezi kushindwa epangwa kuja kunikandamiza ila minasema sina madaraka, fedha na mashahidi ambao nilikuwa nategemea waje kunitolea ushahidi wananipiga chenga kwasababu wapo karibu sana na mzee mwinyi….kikubwa hapa naomba mahakama initendee haki ‘alidai Mzombe huku akiangua kilio.

Mzombe ambapo wakati akitoa utetezi wake alikuwa akiangua kilio na kulitaja jina la Mungu wake, alidai kuwa ameanza kufanya kazi za Mwinyi tangu mwaka 1996 na kwamba Mwinyi amekuwa akimuamini mno na kwamba hakukuwa na mshahara maalumu aliokuwa akilipwa na Mwinyi kwani Mwinyi alikuwa akimchukulia kama mwanae.
“Mzee Mwinyi aliniamini sana na hata mambo mengine ambayo amekuwa akituma nifanye siwezi kuyasema hapa mahakamani kwani hata watoto wake hakuwai kuwashirikisha …mzee hizo nyumba mbili mnazodai leo eti mimi nimemuibia kiasi hicho cha fedha si kweli kwani huyu mzee Mwinyi amekuwa akinipa zaidi ya Sh.milioni 300  niende nikamnunulie majumba, mashamba, nikamjengee majumba naninazipokea mamilioni hayo ya fedha tena bila kuniandikisha sehemu naenda kulipa kwa wahusika na kisha nanunua majumba na hayo mashamba na kuandika jina la Mwinyi.

“Hivi wewe mwendesha mashtaka naomba nikuulize, unaujua husiano wetu na Mwinyi  wewe au unaongee?usitake niseme mengi hapa..hivi unafahamu kuwa Mwinyi nilishakaa na Mwinyi tukajifungia na kuongea na kukubaliana kwamba ninavyomfanyia shughuli zake hizo kwa uaminifu tena bila hata watoto wake hawajui kwamba ipo siku ataninunulia nyumba lakini hadi leo hiyo nyumba hajaninunulia:

“Sasa uenda kesi hii ndio hayo malipo ya kutaka kuninunulia nyumba ambayo aliyoniadi akaamua kunizulia janga hili la kesi tena nimekuja kukamatwa siku ya tatu hapa dar es Salaam,tangu nitoke kijijini Kwetu Songea kumzika mama yangu mzazi na huyo Mwinyi anamfahamu fika mama yangu’alidai Mzombe huku akiangua kilio.
Kuhusu wizi wa fedha za kodi nyumba hizo za Mikocheni na Msasani ambazo ni jumla ni Mil.37, Mzombe alisema kwanza anashangazwa na tuhuma hizo kwani ni rais Mwinyi ndiye aliyempa hela za kwenda kumnunulia nyumba hizo nay eye mshtakiwa akaenda akazitafuta akazinunua yeye mshtakiwa kwa jina la Mwinyi na kisha Mwinyi akajakuzikagua na akampa maelekezo kuwa nyumba hizo ni kwaajili ya kuwapangisha watu na kwamba akampa maelekezo kuwa ukarabati wa nyumba hizo utafanywa na kodi za wapangaji wenyewe na kwamba yeye mshtakiwa ndiye atakuwa msimamazi.

Alieleza kuwa yeye ndiye aliyeenda kuwatafuta madalali na kuwapa kazi ya kutafuta wapangaji na kwamba nyumba ya mikocheni iilikuwa na wapangaji wa nane na kila mmpangaji anapotoa kodi ,basi kodi ile anaenda kumuonyesha mzee mwinyi na mwinyi anampa idhini ya kuendelea na ukarabati katika eneo la mpangaji husika na kwamba fedha zilizokuwa zikisalia anamrudishia mwinyi na kwamba alikuwa hawezi kumshinikiza Mwinyi waandikishiane  kwani Mwinyi alikuwa akimchukulia kama mwanae .

Na kwamba ndiyo maana katika kodi ya nyumba ya Msasani iliyolipwa katika awamu ya tatu ambacho ilikiwa ni sh.milioni sita ,mwinyi alimpatia ili aweze kuongezea kununulia gari lake binafsi la kutembelea lakini hata hivyo gari hilo limegongwa kwa sasa.

“Naomba mahakama itambue, Mwinyi alikuwa akinichukulia kama mwanae na familia yake inanifahamu na hata watoto wake wakitaka kununua mashamba walikuwa wananitumia mimi naenda kuwatafutia mashamba wananipa fedha naenda kuwanunulia naandika majina yao…ndiyo maana hakuna mahali popote panapoonyesha mwinyi alikuwa ananilipa mshahara kiasi gani au aliniajiri, Mwinyi alinichukulia kama mtoto wake licha kuna baadhi ya mambo alikuwa akinishirikisha mimi na watoto hawajui….nitaendelea kumheshimu ila  sijamuibia na mungu ananiona na kwakuwa mimi sina fedha, sina madaraka naomba mahakama hii initendee haki na sikusudii kuleta mashahidi kwani mashahidi niliyokuwa nimepanga kuwaleta wananikwepa kwasababu mashahidi hao wapo karibu na mzee mwinyi hivyo naomba kufunga ushahidi wangu’alidai Mzombe huku akiangua kilio.

 Baada ya kusema hayo hakimu Dudu alisema hukumu ya kesi hiyo ataitoa Februlia  12 mwaka huu, na kwamba kesi hiyo itakuja kwaajili ya kutajwa Januari 24 mwaka huu.

Oktoba 9 mwaka jana, rais All Hassan Mwinyi alifika mbele ya Hakimu Dudu na kutoa ushahidi wake lakini hata hivyo wanausalama ambao walikuwa wakimlinda waliwazuia waandishi wa habari kuingia ndani ya chumba cha mahakama kumuona au kusikiliza ushahidi uliokuwa ukitolewa na Mwinyi lakini jana waandishi wa habari tuliruhusiwa kuingia kusikiliza kesi hiyo.
Kwa mujibu wa hati hiyo ya mashitaka ambayo waandishi wa habari za mahakama walifanikiwa kuipata mahakamani hapo jana ,upande wa Jamhuri unadai  Mzombe anadaiwa kufanya makosa hayo kinyume na kifungu cha 258 na 273 (b) (e) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Sura ya 16 ya mwaka 2002.
  
Siku hiyo ya Agosti 21 mwaka huu, ilidaiwa  kuwa  kati ya Januari Mosi, mwaka 2011 na Julai 2012 huko Mikocheni ,  Mzombe akiwa Wakala wa rais huyo mstaafu, alimwibia  Sh 17,640,000  ambazo ni pato la kodi ya nyumba yake  iliyopo eneo la Mikocheni  wilaya ya Kinondoni.
 
Iliendelea kudai kuwa kiasi hicho cha fedha ambacho Mzombe alimwibia rais Mwinyi kilikuwa ni kodi ya pango la nyumba namba 481,  iliyopo kwenye ploti A ,huko Mikocheni ya mwaka 2011/2012 na 2012/2013.
 
Aidha Mbali anadaiwa kuwa  kati ya Januari Mosi, mwaka 2011 na Julai 10, mwaka huu huko Msasani Village  wilaya ya Kinondoni, mshtakiwa  huyo alimwibia tena rais huyo mstaafu Sh 19,800,000  ambayo ilikuwa ni kodi ya nyumba namba 55 iliyopo kwenye Kitalu C .
 
Iliongezwa kudaiwa kuwa kiasi hicho cha fedha kilikuwa ni kodi ya pango la nyumba hiyo la mwaka  2011/2012 na 2012/2013, hata hivyo mshitakiwa huyo alikana mashitaka yote  na yupo rumande hadi oktoba 22 mwaka,itakapokuja kuendelea kusikilizwa. 

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Januari 11 mwaka 2013
ch 

No comments:

Powered by Blogger.