Header Ads

MAHAKAMA YAMFUNDISHA SHERIA MTUHUMIWA WA KUMJERUHI DK.ULIMBOKA



Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemweleza mtuhumiwa anayedaiwa kumteka na kumjeruhi aliyekuwa Kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk.Steven Ulimboka, Joshua Mulundi  kuwa mamlaka hiyo haina mamlaka ya kuilishinikiza Jeshi la Polisi likamilishe  upesi upelelezi wa kesi hiyo na kesi nyingine.

Kauli hiyo ilitokewa jana na Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Ilvin Mugeta  dakika chache baada ya Mulundi ambaye ni raia wa Kenya kumuomba Hakimu mkazi anayesikiliza kesi yake Agnes Mchome  amruhusu akamuone Mugeta ili amueleze matatizo yake hayo ambayo awali alishamweleza hakimu Mchome.
Itakumbukwa kuwa jana kesi ya Mulundi ilikuwa imekuja kwaajili ya kutajwa mbele ya Hakimu Mchome na wakili Mwandamizi Tumaini Kweka aliambia mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na hakimu huyo akaiarisha hadi Januari 23 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na kuamuru mshtakiwa arudishwe rumande.

Baada ya Kweka kutoa maelezo hayo mbele ya Hakimu Mchome, ndipo Mulundi aliomba ruhusa aongee ndipo akaanza kumueleza hakimu huyo kuwa yeye hivi sasa yupo kwenye mgomo wa kutokula kwasabababu anashindwa kuelelewa ni kwanini upande wa mashtaka unachelewa kukamilisha upelelezi na kwamba anataka balozi wa Kenya nchini hapa afike mahakamani.

Hata hivyo hakimu Mchome alisema ameyasikia madai yake ila kwa mujibu wa sheria mahakama ya Kisutu  haina mamlaka ya kusikiliza kesi yake na kwamba mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi yake ni Mahakama Kuu .
“Kama ni hivyo basi naomba hakimu Mchome unipe idhini niende kumuona kiongozi wako(Mugeta)’aliomba Mulundi.
Ombi ambalo lilikubaliwa na hakimu Mchome ambapo askari magereza walimsindikiza mshtakiwa huyo hadi ofisini kwa hakimu Mugeta ambapo alifika na kuanza kumueleza madai hay ohayo hayo aliyiokuwa amemweleza hakimu Mchome na kwamba anaomba Mugeta  amuite balozi wa Kenya mahakamani na awalazimishe upande wa mashtaka umalize upelelezi wao.

Hata hivyo hakimu Mugeta akimjibu mshtakiwa huyo alisema hivi ; “mahakama haina mamlaka ya kulishinikiza jeshi la polisi likamilishe upelelezi  na kwamba kuna taratibu zinatakiwa zifuatwe za kumuita balozi wan chi husika kuja mahakamani”alisema hakimu Mugeta na mshtakiwa huyo akarudishwa rumande.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Januari 11 mwaka 2013

No comments:

Powered by Blogger.