Header Ads

MASHAHIDI WAKWAMISHA KESI YA VIGOGO SUMA JKT


Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA  ya Hakimu  Mkazi Kisutu Dar es Salaam,jana ilishindwa kuanza kusikiliza kesi ya  inashindwa kuanza kusikiliza KESI ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili Mkurugenzi wa Shirika la Kujenga Taifa (SUMA JKT), Kanali Ayoub Mwakang’ata na maofisa wengine wa jeshi hilo kwasababu shahidi wa upande wa jamhuri aliyetarajiwa kuja jana kutoa ushahidi ameshindwa kufika mahakamani hapo kwasababu amesafiri.

Hakimu Mkazi Alocye Katemana alisema kesi hiyo ilikuwa imekuja kwaajili ya mashahidi wa upande wa jamhuri kuanza kutoa ushahidi wao ,lakini wakili wa upande wa Jamhuri ameiomba mahakama hiyo iarishe hadi tarehe nyingine kwasababu shahidi waliyekuwa wamemuanda ajae kutoa ushahidi amesafiri.

“Kwa sababu hiyo mahakama hii inaairisha kesi hii hadi  Machi 4 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya mashahidi wa jamhuri kuanza kutoa ushahidi wao”alisema Hakimu Katemana.
Mbali na Kanali Mwakang’ata washitakiwa wengine ambao walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza na TAKUKURU, Julai 2 mwaka jana , ni Luteni Kanali Mkohi Kichogo,Luteni Kanali Paul Mayavi,Meja Peter Lushika,Sajenti John lazier,Meja Yohana Nyichi na Mkurugenzi wa Miradi ya Matrekta wa SUMA JKT-Luteni Kanali Felex Samillan wanaotetewa na wakili wa kujitegemea Majura Magafu.

Wanakabiliwa na makosa ya kula njama na matumuzi mabaya ya madaraka kuwa washitakiwa wakiwa ni wajumbe Ilidai kuwa Machi 5 mwaka 2009 katika chumba cha mikutano cha ofisi ya SUMA JKT Dar es salaam,wakiwa ni wajumbe wa bodi na Bodi ya Tenda ya SUMA JKT kwa makusudi walitumia madaraka yao vibaya kwa kutoa maamuzi ya bodi hiyo ambayo yaliyoonyesha yametolewa na TAKOPA kwa madhumuni ya kununua magari na vifaa vya ujenzi bila kupata idhini ya kutoka Bodi ya ya Wakurugenzi ya TAKOPA. 

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Januari 30 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.