Header Ads

KG.210 ZA PEMBE ZA NDOVU ZAWAFIKISHA KIZIMBANI


Na Happiness Katabazi

WATU wanne jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na makosa mawili ya kumiliki Kg.210 za Pembe za Ndovu bila kibali na kusaidia washitakiwa kutenda kosa.

Wakili wa serikali Hamidu Mwanga mbele ya Hakimu Mkazi Stewart Sanga aliwataja washitakiwa hao kuwa Peter Kabi,Leonida Loi Kabi, Charles Wainaina na Polisi Malisa.

Wakili Mwanga alidai shitaka la kwanza kwaajili ya washitakiwa wote ni  la kukutwa wakimiliki nyara za serikali kinyume na kifubgu cha 86(1), 2(2) na 3 cha Sheria Uhifadhi wa Wanyapori  Na.5 ya mwaka 2009  kinachosomwa pamoja na  kifungu cha 57(1) na mstari  wa 14(d) katika jedwali la kwanza pamoja na sheria Economic And Organazation Crime Control Act ya mwaka 2002.

Kuwa Novemba 11 mwaka huu, huko eneo la Kimara Dar es Salaam walikutwa wakimiliki  pembe za Ndovu  zenye uzito wa Kg.210 zenye thamani ya dola za Kimarekani 247,830,000 ambazo wakati huo  zilikuwa na thamani  ya Sh 391,571,400 na vipande vitano vya mifupa ya Tembo zenye thamani ya dola za Kimarekani  30,,000,000 wakati huo  zilikuwa na thamani ya sawa na Sh 47,400,971,400 mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila leseni.

Wakili Mwanga alidai shitaka la pili ni kwaajili ya mshtakiwa wa tatu na wanne(Charles Wainaina na Polisi Malisa) , ambalo ni la kuwasaidia washitakiwa kutenda kosa kinyume na kifungu cha  387 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, ambapo alidai kuwa Wainaina na Malisa kuwa Oktoba 27 mwaka huu,  huko katika Kituo cha Polisi Kimara  huku wakijua kuwa mshitakiwa wa pili(Leonida Loi Kabi)  alikuwa amekamatwa kwa tuhuma za kukukutwa akimiliki mali  nyara za serikali , alimsaidia Kabi kwa kuwashawishi  polisi  kwa lengo la kumuweza Kabi atoroke ili asiadhibiwe, na kwamba upelelezi bado haujakamilika.

Hata hivyo washtakiwa wote walikanusha mashtaka hayo na hakimu Sanga alisema jana hawezi kutoa masharti ya dhamana na akaamuru washitakiwa wapelekwe rumande hadi Novemba 12 mwaka huu, ambapo siku hiyo ndiyo atatoa masharti ya dhamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Agosti 9 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.