Header Ads

VIONGOZI MTAA WA KIBASILA KORTINI KWA UHUJUMU UCHUMI


Na Happiness Katabazi

VIONGOZI wawili wa serikali ya mtaa wa Kibasila jijini Dar es Salaam na Mfanyakazi wa Benki ya NMB, tawi la Kibasila wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  wakikabiliwa na mashtaka 41, likiwemo la uhujumu uchumi na wizi wa Sh.Milioni 18.6 mali ya serikali  ya mtaa wa Kibasila.
 
Mbali na mashtaka hayo, pia wanakabiliwa na mashtaka ya kughushi, matumizi mabaya  ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri  wao na wizi wakati wakiwa watumishi wa Umma.
Waendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Salha Abdallah na Sophia Gulla mbele ya Hakimu  Bingi Mashabala waliwataja washitakiwa hao kuwa ni  Mwenyekiti  wa Serikali ya mtaa wa Kibasila, Aboubaker Maddy, Katibu wake, Stephen Mtangi na mfanyakati wa benki ya NMB tawi la Muhimbili, Dorca Mtaita na kudai kuwa washtakiwa hao walitenda makosa hayo kati ya Mei 13, mwaka 2006 na Desemba 10, mwaka 2008.
 
Wakili huyo alidai kuwa  mshtakiwa Maddy na Mtangi wakiwa  ni waajiriwa wa serikali  ya Mtaa wa Kibasila  na kwamba walitumia dhamana ya serikali  waliyopewa kudanganya wakubwa wao  kwa kutumia hati ya benki ya Desemba 10, 2008 kuonyesha maelezo ya uongo ya akaunti namba  SA 2092502906 ya NMB tawi la Muhimbili.
 
Aidha mawakili hao wa Takukuru walidai kuwa pia washtakiwa hao walitenda kosa kuisababishia serikali ya Mtaa wa Kibasila  ya Sh 18,640,200 kutokana na   kughushi nyaraka kinyume na kifungu cha 333, 335 na 337 vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002.

Kuhusu mfanyakazi wa NMB, Abdallah alidai kuwa  Desemba 10, mwaka  2008 , Dorca  akiwa mwajiriwa katika  benki ya NMB tawi la Muhimbili  alighushi hati ya benki hiyo  na kuonyesha kuwa akaunti ya serikali ya mtaa wa Kibasila yenye namba SA 2092502906 ina Sh 18,009,379.13 wakati akijua kuwa ni uongo na kwamba akufanya hivyo alimsadia  Maddy kutenda kosa.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, washtakiwa wote walikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.
 
Na kwa upande wake Hakimu Mashabala alisema ili kila mshtakiwa apate dhamana ni lazima awe na wadhamini wawili  wenye vitambulisho na barua ambapo kila mdhamini  alitasaini bondi  ya Sh.milioni tatu.Washitakiwa hao waliweza kutimiza masharti hayo na hakimu Mashabala aliwapatia dhamana na akaairisha kesi hiyo hadi Januari 5, mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kutajwa .

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Novemba 22 mwaka 2012.
 

2 comments:

Anonymous said...

Аctually no matter if someοne ԁoesn't know after that its up to other visitors that they will assist, so here it occurs.

My web page Same Day Payday Loans

Anonymous said...

Ηaving гeаԁ this I thought іt was rather
еnlightenіng. I аρpreciаtе you finding the time anԁ effοrt tо put thіs
іnfoгmatіve аrtіcle together.
I oncе agаin find myself personally spending way too muсh timе both reading аnd commenting.
But ѕo what, it was ѕtill ωorthwhіlе!


Fеel freе tο suгf to my web
blog: New Bingo Sites

Powered by Blogger.