Header Ads

MAOFISA WA TAZARA KIZIMBANI

Na Happiness Katabazi

MAOFISA wawili wa TAZARA  jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na makosa mawikili likiwemo la kusababishia TAzara sh milioni 120.

Mbele ya Hakimu Mkazi Frank Moshi wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Mhandisi Mkuu wa Mitambo , Wenceslaus Kamugisha na  Meneja Mkuu wa Fedha wa Tazara, Sarah Masiliso.

Wakili Kweka alidai shtaka la kwanza ni la matumuzi mabaya ya madaraka ambalo ni kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa ya mwaka 2007, kuwa mnamo Aprili mwaka 2011,  wakiwa ni waajiliwa wa kwa nyadhifa hizo  kwa makusudi walitumia madaraka yao vibaya kwa kupitisha maombi katika mchakato wa tenda  kinyume na sheria na kwa malengo ya kuipatia faida kampuni ya Chrinkap Indutrial.

Wakili Kweka alidai kosa la pili ni la kusababisha hasara  ambalo ni kinyume na mstari wa 10(1) ya jedwari la kwanza  na kifungu cha 57(1)  na 60(2) cha Sheria ya Uhujumu uchumi.

Kwamba Aprili  mwaka 2011 katika maeneo ya Ilala jijini Dar es Salaam,  washtakiwa wakiwa ni waajiliwa wa Tanzania, Zambia Lairway Authority  kwa makusudi waliisababishia serikali ya Tanzania hasara y ash 120,000,000.

Hata hivyo washtakiwa hao walikana mashtaka  na hakimu Mosha alisema ili wapate dhamana ni lazima kila mshtakiwa awe  na wadhamini wa wili ambao wanafanyakazi katika taasisi zinazotambulika na serikali  na kwamba wadhamini mmoja  atasaini bondi ya Sh.milioni 10 na kwamba mdhamini mmoja  au mshtakiwa ataweka mahakamani fedha taslimu  sh milioni 30 au hati ya mali isiyoamishika yenye thamani hiyo ya milioni 30.

Lakini hata hivyo mdhamini mmoja aliwasilisha hati ya mali isiyoamishika yenye thamani y ash.milioni 62 ambayo aliomba hati hiyo itumike kuwadhamani washtakiwa wote ombi ambalo lilikubuwaliwa na hakimu hiyo licha wakili Kweka aliomba mahakama iupatie muda upande wa jamhuri uende kuikagua hati hiyo ,na hakimu alikubali hoja hiyo akaiarisha kesi hiyo hadi leo ilikuja kuona kama washtakiwa walikuwa wametimiza masharti hayo ya dhamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 27 mwaka 2012. 

No comments:

Powered by Blogger.