Header Ads

RUFAA YA GODBLES LEMA KUANZA DESEMBA 4



Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Rufani nchini , Desemba 4 mwaka huu, itaanza rasmi kusikiliza  rufaa iliyokatwa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini(Chadema),  Godbless Lema, ya kupinga hukumu ya MAhakama Kuu Kanda ya Arusha ambayo ilimvua ubunge Lema.

Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya Rufani, inaonyesha uongozi wa mahakama hiyo upanga jopo la majaji watatu watakao sikiliza kesi hiyo ambao ni Jaji Salum Massati, Natharia Kimaro na Bernad Luanda ambao kikao kitaketi jijini Dar es Salaam, kuanzia saa tatu asubuhi.

Kupwangwa kwa rufaa hiyo kuanza kusikilizwa tarehe hiyo kumekuja baada ya Lema kuwasilisha rufaa yake upya ambayo ameifanyia marekebisho kama alivyoamliwa na mahakama hiyo Novemba 8  mwaka huu, ambapo mahakama hii ilikataa ombi la wajibu maombi katika rufaa hiyo waliyotaka Mahakama hiyo iifute rufaa ya Lema kwa sababu ina mapungufu badala yake mahakama hiyo ilikiri kuaini mapungufu katika rufaa ya Lema lakini ikasema mapungufu hayo hayawezi kuifanya mahakama ifikie uamuzi wa kuifuta rufaa ya Lema kwani mapungufu hayo yalifanywa na watendaji wa mahakama ambao ndiyo waliandaa rufaa hiyo na ikampatia Lema siku 14 kuanzia siku hiyo awe amewasilisha upya rufaa yake aliyoifanyia marekebisho.

Aprili 5 mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilitoa hukumu yake na kumvua ubunge Lema
Lema  kufuatia kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu  wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, wakipinga ushindi wake katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.

Lakini baadaye, alikata rufaa Mahakama ya Rufani, kupitia kwa wakili wake Method Kimomogoro kupinga hukumu ya Mahakama Kuu, huku akitoa hoja 18 za kupinga hukumu hiyo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 27 mwaka 2012. 

No comments:

Powered by Blogger.