Header Ads

PRO.KAPUYA KULISHTAKI DIRA KWA KUMSINGIZIA KAFICHA FEDHA ZA SERIKALI NJE YA NCHI


Na Happiness Katabazi

WAZIRI wa Mstaafu wa Wizara ya Ulinzi ,Profesa Juma Kapuya  amelitaka Gazeti la Dira limlipe fidia ya bilioni tano na limuombe radhi  ndani ya siku 14 kuanzia sasa ama sivyo atalifikisha mahakamani gazeti hilo kwa kuchapisha habari ya uongo dhidi yake kuwa ameiba fedha za umma na kwenda kuzificha katika benki ya Switzeland  kwasababu habari hiyo imemletea madhara na kumshushia heshima yake.

Profesa Kapuya  kupitia wakili wake Yassin Memba tayari ameishalikabidhi gazeti la Dira kusudio hilo ambapo nakala ya kusudio hilo ambalo gazeti hili linayonakala yake Kapuya anasema  gazeti hilo  linalochapishwa mara moja kwa wiki katika toleo lake Na.207 la Jumatatu  ya Novemba 12-18 ya mwaka huu, lilichapisha habari ya kumkashfu na ndiyo maana analitaka gazeti hilo limuombe radhi ndani ya siku 14 kaunzia sasa.

Wakili Memba alisema habari hiyo iliyomkashfu mteja wake ni ile iliyochapishwa ukurasa wa mbele ambayo ilikuwa na kichwa cha habari kisemacho; “VIGOGO WA MABILIONI YA USWISS HAWA HAPA”.

Alisema kichwa hicho cha habari ambacho kilikuwa kimepambwa na picha ya vigogo hao ikiwemo Picha ya mteja wake (Profesa Kapuya) ambayo ni kama ushahidi wa habari hiyo ambayo ilipandishwa ukurasa wa kwanza, na mstari wa 16,17 na 18 ambazo zilikuwa zikisomeka kama ifuatavyo:

“Zitto  alieleza zaidi kuwa  wengine ambao mali zao  zinapaswa  kuchunguzwa  kwa kina  na Serikali ni waliopata kushika  wadhifa  wa uwaziri  wa ulinzi  na ukuu wa majeshi  katika kipindi  hicho  cha mwaka  2003 hadi 2010.

“Mawaziri waliopata  kuiongoza  Wizara ya Ulinzi  katika kipindi  hicho  ni pamoja  na Profesa  Philemoni Sarungi, Profesa Juma Kapuya  na Edgar Maokola Majogo na wakuu wa Majeshi  walikuwa Jenerali Robert Mboma na Jenerali  Geogre Waitara. Majina ya vigogo  jawa waliopata kuongoza  wizara ya ulinzi  katika serikali ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa yanaingia  katika mlolongo wa majina yanayotakiwa na Zitto kufanyiwa uchunguzi  wa kina  wa mali zao  na Serikali  kutokana  na kuwa  madarakani  wakati  kampuni  ya Meremeta  ambayo baadaye  ilibadilishwa  jina kuitwa  TanGold iliyokuwa  ikifanyakazi  chini ya Jeshi kudaiwa kutorosha mabilioni  ya fedha nje ya nchi”.

Wakili Memba alisema mstari Na. 28 wa habari hiyo ulikuwa na maneno yanayosomeka hivi; “Fedha  zilizoibwa na kutoroshwa  kupitia kampuni ya Meremeta  na kampuni ya Deep green ziliishia kwenye akaunti  za watu  binafsi  nje ya nchi.Hata hivyo  mara baada  ya kuundwa  kwa kampuni ya TanGold, jumla  ya dola  za Kimarekani  milioni 10 ziliwekwa kwenye akaunti  ya kampuni  hiyo  katika Benki ya NBC, Tawi la Corporate .Nambari  ya akaunti hiyo  poa itatolewa katika kamati  ninayoomba  kuunda  kwa ajili ya uchunguzi wa kina”.

“Hayo maneno yaliyochapishwa kwenye hiyo habari kuhusu Kapuya ambaye alikuwa Waziri wa Ulinzi wa zamani kuwa aliamisha fedha za serikali kinyume cha sheria na kwenda kuzificha katika benki huko nchini Switzerland, na habari hiyo ya uongo ilikuwa na lengo la kumchafulia jina mteja wangu na kumshushia heshima yake  na kumchonganisha na wananchi  na imemletea madhara ya kiafya na kumsababishia usumbufu mkubwa   na tangia ilipochapishwa hiyo habari mteja wangu anataka gazeti lako limlipe Sh.bilioni tano kama fidia ya madhara aliyoyapata tangu habari hiyo ilivyochapishwa”alisema Wakili Memba.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Novemba 28 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.