Header Ads

WATUHUMIWA WA UVUVI WA MELI HARAMU WACHARUKA MAHAKAMANI

Na Happiness Katabazi

RAIA 32 wa kigeni ambao Machi mwaka huu, walikamatwa kwenye meli ya Tawariq 1 wakifanya uvuvi haramu katika Bahari ya Hindi ambao wanakabiliwa na kesi ya uvuvi haramu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana walicharuka mahakamani hapo na kutishia kuanza mgomo wa kutokula chakula.


Hali hiyo ambayo haikutarajiwa ilitokea jana mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema, ikiwa ni takribani sekunde chache tangu hakimu huyo aseme kuwa hataweza kuandika kurekodi chochote kwasababu jarada la kesi ya washitakiwa bado lipo Mahakama Kuu na kwamba anaairisha kesi hiyo hadi Juni 23 mwaka huu, na wakili wa serikali Rose Chilongola kuanza kuondoka

Baada hakimu huyo kusema hayo washitakiwa wote walinyosha vidole juu huku wakisema kwa lugha ya Kiingereza kama ilivyotafrisiliwa na gazeti hili kwa lugha ya Kiswali‘no no no’.

“Tangu mapema Machi mwaka huu tupo rumande hakutajapa dhamana wala kutolewa uamuzi wa vigezo gani tutizimize tupate dhamana sisi tunateseka,hatutendewi haki na nchi hii kwani hata kama kweli tumekamatwa tunavua samaki kwenye ardhi ya Tanzania bila kibali tunaomba tupatiwe dhamana ili tuweze kufanya mambo mengine kwani sisi pia tuna haki ya kupata dhamana kwa wakati.Na tumeamua sisi sote washitakiwa kuwa kitu kimoja hadi haki itendeke’alidai mshitakiwa huyo.

Na kwa upande wa wakili wa washitakiwa ho Elias Nawela alidai kuwa anashangazwa hadi kufikia jana jarada la kesi kutokuwa limefika Mahakama ya Kisitu kwani tayari Mahakama Kuu ilishalitolea uamuzi.

Hata hivyo Lema baada ya kusikiliza malalamiko ya washitakiwa hao ambao awali walidai hawafahamu lugha ya Kiingereza lakini jana waliitumia kufikisha kilio chao, alisema anawaidi atakapomaliza kusikiliza kesi alizokuwa akizikiliza jana atafuatilia jarada hilo Mahakama Kuu.

Mei mwaka huu, upande wa mashitaka katika kesi hiyo ulipeleka jarada la kesi hiyo Mahakama Kuu, ili mahakama hiyo iamuru samaki hao wauzwe au la , Jaji Gerofrey Shaidi katika uamuzi wake kuhusu ombi hilo alisema hilo siyo jukumu la mahakama na kuwa jukumu hilo ni la Maofisa Uvuvi.

Washitakiwa hao ni mabaharia, Jiojwen Chang (34), Jia Yin Zhao 26), Gexi Zhao (36), Zongmin Ma (36), Dong Liu (25), Yongiao Fang (22), Nguyen Tuan(23), Hsu Sheng Pao (55), Zhao Hanquing (39), Zho Hanging (39) ambaye wote ni wakala na raia wa China.

Wengine ni Tran Van Phuon (33), Pham Dinn Suong (31), Tran Van Thanh (23), Cao Vuong (27), Kristofer Padilla (29) raia wa Vietnam. Wengine ni Mohamed Kiki (61), Anul Mani (24) raia wa Taiwani.

Aidha, Wakili Mganga alisema washtakiwa wengine ni Jejen Priyana (22), Kuntoto Suratno (27), Tusi Ame (25), Ifan Herman Pandi (21), raia wa Indonesia, Silvano Garanes (32), Benjie Rosano (34), Ignacio Dacumos (31), Marlon Maronon (33), Jhoan Belano (34), Rolando Nacis (35) raia wa Philipins, Wakati Ali Ali Mkota (32), Juma Juma Kumu (40), Jackson Toya(39) raia wa Kenya.

Machi 10 mwaka huu, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washtakiwa wote wanakabiliwa na mashtaka mawili, shitaka la kwanza ni kuvua samaki bila leseni kinyume na sheria ya Uvuvi wa Samaki katika kina kirefu ya mwaka 2009.

Alidai Machi 8 mwaka huu, washtakiwa wote kwa pamoja, saa sita usiku katika ukanda wa bahari ya Hindi ndani ya eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walikamatwa wakiwa wakivua samaki bila leseni.Na washtakiwa wote walikana mashtaka na wapo rumande kwaajili ya wameshindwa kutimiza masharti dhamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Julai 11, 2009

No comments:

Powered by Blogger.