Header Ads

DK.BILAL AMPOZA MUDHIHIR

Na Happiness Katabazi, Lindi

MGOMBEA mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Garib Mohamed Bilal, amempoza machungu aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Mchinga aliyeangushwa katika kura za maoni, Mudhihir Mudhihir.


Akihutubia mkutano wa kampeni katika Kijiji cha Kilangala mkoani hapa jana, Dk. Bilal hakusita kummwagia sifa mbunge huyo wa zamani kwa ushujaa wake wa kujitokeza na kumuunga mkono mpinzani wake.

Mudhihir amekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa vipindi vitatu, ambapo awali ilidaiwa kudondoshwa kwake kulitokana na kutoelewana kwake na Mbunge wa Mtama, ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe.

“Sisi katika CCM hatuna tabu, hata kama kuna vita ndani yetu tunaimaliza baada ya uchaguzi…na kwasababu hiyo makundi yamekwisha, kwahiyo natangaza rasmi kwa moyo mmoja, nitamuunga mkono mgombea ubunge wa sasa na nitahakikisha anapata ushindi wa kishindo,” alisema Mudhihir huku akimalizia hotuba yake kwa kuimba wimbo.

Dk. Bilal alisisitiza kwa kuwataka wanachama wa chama hicho kumaliza makundi haraka iwezekanavyo, alisema siku zote panapokuwepo makundi yanayohasimiana ndani ya chama, ni wazi chama hicho kinaweza mara kwa mara kujikuta kinaingia kwenye migogoro isiyo na tija.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamis, Agosti 26 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.