Header Ads

JAMHURI YAKWAMISHA KESI YA JAMHURI

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, jana ilishindwa kuanza rasmi kusikiliza ushahidi wa upande wa Jamhuri katika kesi ya tuhuma za kughushi na kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa serikali inayomkabili Naeem Adam Gile kwasababu upande wa jamhuri ulishindwa kuleta mashahidi wake.

Gile anadaiwa kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma na kwamba Julai 20, 2004 eneo la Ubungo Umeme Park, alitoa taarifa ya uongo kwa wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Shirika la Umeme (TANESCO). Kwamba Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa Tanzania ili wajumbe wa bodi hiyo waweze kumpendekeza kupewa tenda ya kutoa huduma hiyo.

Mbele ya Hakimu Mkazi Walirwande Lema, Wakili Serikali Fredrick Manyanda aliikumbusha mahakama kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa ila kwa bahati mbaya hawakuwa wameleta mashahidi na hivyo kuomba iarishwe.

Kwa upande wake wakili wa mshtakiwa, Alex Mgongolwa aliiomba mahakama iuamuru upande wa Jamhuri ile mashahidi kama inavyokuwa imeamuriwa na mahakama kwani kesi hiyo ni ya muda mrefu.Hakimu Lema aliairisha kesi hiyo hadi Machi 24 mwaka huu, na itakuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa.

Wakati huo huo Kesi ya Uhujumu ya Euro milioni mbili inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia na Grace Martin jana walishindwa kuanza kujitetea kwasababu Jaji Sivangilwa Mwangesi anayesikiliza kesi hiyo kutotokea mahakamani lipa upande wa Jamhuri na Utetezi kuwa tayari kuendelea na kesi hiyop , hali iliyosababisha Hakimu Mkazi Mustapher Siyani kuiarisha hadi Machi 25 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kuanza washtakiwa kuanza kujitetea.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Februali 25 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.