Header Ads

KESI YA RICHMOND SASA KUUNGURUMA FEBRUALI 24

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam,Februali 24 mwaka huu, itaanza rasmi kusikiliza kesi ya tuhuma za kughushi na kutoa taarifa za uongo kwa watumushi wa serikali inayomkabili Naeem Adam Gile.

Wakili wa Serikali Shadrack Kimaro mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema alieleza kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kutajwa na kwamba upande wa Jamhuri upo tayari kwaajili kuanza kusikilizwa.

Hakimu Mkazi Lema alisema anakubaliana na ombi hilo na anaiarisha kesi hiyo hadi Februali 24 mwaka huu, kesi hiyo ambapo itakuja kwaajili ya mashahidi wa upande wa Jamhuri kuanza kutoa ushahidi wao.

Awali Janurai 13 mwaka 2009, ilidaiwa mahakamani hapo na Wakili Mkuu wa Serikali, Stanslaus Boniface kuwa mshtakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka matano ambayo aliyatenda kwa nyakati tofauti.

Wakili Boniface alidai kuwa, Machi 13, 2006, jijini Dar es Salaam, mshitakiwa akiwa na dhamira ya kutenda kosa, alighushi hati ya nguvu ya kisheria (power of attorney) inayoonyesha imetolewa na Hamed Gile, ambaye ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, kwamba amemruhusu kufanya shughuli za kampuni hiyo hapa nchini.

Wakili Boniface alidai kwamba, shitaka la pili ni kutoa taarifa za uongo, kuwa Machi 20 mwaka 2006, katika eneo la Ubungo, Umeme Park, Barabara ya Morogoro, mshitakiwa alitoa hati hiyo ya nguvu ya kisheria inayomuidhinisha yeye kwamba ameruhusiwa kufanya kazi ya kampuni hiyo ya Marekani hapa nchini.

Aliendelea kudai kuwa, shitaka la tatu linalomkabiri mtuhumiwa huyo ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma na kwamba Julai 20, 2004 eneo la Ubungo Umeme Park, alitoa taarifa ya uongo kwa wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Shirika la Umeme (TANESCO). Kwamba Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa Tanzania ili wajumbe wa bodi hiyo waweze kumpendekeza kupewa tenda ya kutoa huduma hiyo.
Katika shitaka la nne, alidai Juni, 2006 jijini Dar es Salaam, mshitakiwa alitoa taarifa za uongo kwa wajumbe wa timu ya majadiliano ya serikali, kuwa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme kwa kiwango hicho ili apewe tenda hiyo.

Aidha alidai shitaka la tano alinadaiwa kulitenda Julai, 2006, ambapo mshitakiwa akifahamu na kwa ulaghai, alitoa hati ya nguvu ya kisheria iliyotolewa Machi 3, mwaka huo iliyokuwa ikimuonyesha kuwa ameruhusiwa na Mwenyekiti wa Kampuni, Hemed Gile, kufanya kazi za kampuni hiyo hapa nchini.

Gile alifikishwa mahakamani hapo ikiwa ikiwa ni siku chache baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na mwenzake aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, walilazimika kujiuzuru nyadhifa zao kwa kashfa hiyo ya Kampuni ya Richmond.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumapili, Februali 10 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.