Header Ads

MPENDAZOE AKWAMA KORTI KUU

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali ombi la aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea(CHADEMA), Fred Mpendazoe lililokuwa linaiomba mahakama hiyo imsamehee kulipa shilingi milioni 15 za kesi yake ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambayo yalimtangaza Naibu wa Kazi na Ajira, Dk.Makongoro Mahanga (CCM) kuwa ndiye mbunge wa jimbo hilo kwasababu lina dosari za kisheria.

Katika kesi ya msingi ya kupinga ubunge wa jimbo hilo iliyofunguliwa mahakamani hapo mwishoni mwa mwaka jana na Mpendazoe na ambayo bado haijaanza kusikilizwa wadaiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk.Mahanga na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo.Na Mdaiwa anaomba mahakama hiyo itengue ubunge wa mdaiwa wa pili (Dk.Mahanga) anayetetewa na wakili wa kujitegemea Jerome Msemwa.

Uamuzi wa ombi hilo la kuomba mahakama imsamehe kulipa gharama za kesi ya uchaguzi ulitolewa jana na Jaji Profesa Juma Othman ambaye alisema baada ya kupitia kwa kina ombi hilo amebaini hati ya kiapo iliyoambatanishwa na ombi hilo lina dosari za kisheria na kwasababu hiyo analitupilia ombi hilo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 inamtaka mlalamikaji katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge aliweke Mahakama Kuu shilingi milioni tano kwa kila mtu anayemlalamikia.Na Kwenye Kesi hiyo Mpendazoe anapaswa aweke mahakamani jumla ya Sh milioni 15 kwababu anawalalamikia wadaiwa watatu ambao ni Mwanasheria Mkuu wa Seriakali, Dk.Mahanga na Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Segerea.

Aidha Jaji Othman aliairisha kesi hiyo Februali 23 mwaka 2011 kesi ya msingi itakapokuja kwaajili ya kutajwa na kuangalia mlalamikaji kama tayari ameishaweka weka kiasi hicho cha fedha mahakamani ili mahakama hiyo iweze kupanga tarehe ya kuanza kusikiliza kesi hiyo ya msingi iliyofunguliwa na Mpendazoe.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Februali 16 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.