Header Ads

WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA FREE MEDIA LTD ,WAKIUKARIBISHWA MWAKA 2011 KWA KISHINDO

Happiness Katabazi ambaye ni mwandishi wa habari mwandamizi akigonganisha glasi na mgeni rasmi katika sherehe hiyo, Freeman Mbowe.

****************************************************
Mbowe aiongezea mtaji Free media Saccos
Mwenyekiti wa makampuni ya Bilicanas Co.Group na Freemedia Ltd, Freeman Mbowe, ameahidi kutoa mtaji wa kutosha kwa kila mfanyakazi kwa ajili ya uanzishwaji wa “Freemedia Saccos” inayolenga kutoa fursa zaidi za mikopo kwa wafanyakazi wa kampuni hizo.
Mbowe aliyasema hayo usiku wa kuamkia jana wakati wa sherehe maalum ya kuukaribisha mwaka 2011 na kupongezana ambazo ziliandaliwa kwa pamoja na viongozi wa kampuni hizo wakiwemo wale wa Freemedia Ltd inayochapisha magazeti ya Tanzania Daima na Sayari.
Katika shughuli hiyo, Mbowe aliwaomba wafanyakazi kuendelea kujituma pamoja na kukabiliana na ushindani wa kibiashara sambamba na kuhakikisha wanafanikiwa kuendesha maisha yao kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya kujipatia kipato.
“Kilio chenu nimekisikia, ni hakika wakuu wenu wa idara wanakamilisha taratibu zote ili kuondoa matatizo yaliyopo, na jambo la msingi ni uwepo wa SACCOS, nimelipokea na nawaahidi nitawasaidia kwa hali na mali,” alisema Mbowe.
Alisisitiza kuwa atatoa wataalam wa kushughulikia suala hilo na mtaji wa kutosha kwa SACCOS hiyo.
Katika shughuli hiyo wafanyakazi kutoka idara zote za makampuni hayo matatu walikutana kwa pamoja na familia zao na kuweza kubadilishana mawazo pamoja na kusherehekea.


Nuru Yanga,Hadija Kalili, Dina Ismail na Iren Mark wakifurahia
Nikienda kugonganisha glasi ya mvinyo na wenzangu

No comments:

Powered by Blogger.