Header Ads

MASHAHIDI WAZIDI KUMNYOSHEA VIDOLE SHEIKH PONDA


Na Happiness Katabazi
FUNDI mwashi Hamis Salum Mkangama(30), ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa Oktoba  7 mwaka jana, mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya uchochezi na wizi wa malighahfi zenye thamani ya  Sh.milioni 59 inayomkabili  Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Issa Ponda Issa na wenzake 49 aliwataka wasimamishe ujenzi wa ukuta wa kutenganisha kiwanja cha Markas kilichopo Chang’ombe na Msikiti.
Mkangama ambaye ambaye ni shahidi wa sita wa upande wa jamhuri alitoa madai hayo jana mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa wakati akiongwa na wakili Mwanadamizi wa serikali Tumaini Kweka kutoa ushahidi wake.
Mkangama alieleza kuwa yeye ni fundi mwashi ambaye ambaye anatengeneza matofali na kwamba Oktoba 7 mwaka jana  yeye na wenzie 20 walikuwa katika kiwanja cha Chang’ombe Markas kinachomilikiwa na kampuni ya Agritanza Ltd akijenga ukuta unaotenganisha kiwanja cha Chang’ombe Markas na Msikiti na kwamba walikuwa katika hatua ya kuchimba msingi.
“Ghafla ilipofika saa 10 jioni alikuja Ponda na akatuuliza nani katuruhusu tujenge ukuta katika kiwanja hicho, tukamjibu ni Suleiman ambaye ni bosi wetu, Ponda akatutaka tusimamishe ujenzi haraka  kwani eneo hilo bado lina mgogoro ,sisi tukamjibu  hatuwezi kusimamisha ujenzi  hadi bosi wetu Suleiman aliyetupa kazi hiyo atukataze, sisi tutaendelea na ujenzi:
“Ponda akaamua kuachana na sisi wajenzi akaanza kupiga picha hilo eneo la kiwanja cha Markas  ambalo tulikuwa tunajenga ukuta  alipomaliza kupiga picha  akatoe mlinzi  wa eneo lile  ambaye alikuwa hamfahamu Ponda  wakanza kujibishana  na Ponda   kisha mlinzi Yule akaamua kumjulisha bosi wake kwa njia ya simu kuhusu ujio wa Ponda  na bosi yule akaja akatutaka tusieendelee na ujenzi kwani endapo tutaendelea kuna matatizo yanaweza kutokea na akatueleza kuwa yeye anaenda kuripoti ujio huo wa Ponda katika vyombo vya dola”alidai Mkangama.
Kwa upande wake Shahidi wa saba,  William Milanzi(43) ambaye  ni mlinzi wa eneo linalopakana na kiwanja cha Markas ambapo alidai amewekwa kufanya kazi hiyo na mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Seif  ambaye ndiye aliyempa jukumu la kulinda pia eneo la Suleiman ambalo ni la kiwanja cha Markas kwaajili ya kulinda malighafi zilizokuwa zimeifadhiwa pale ambazo ni matofali, mbao, nondo na malighafi nyingine nyingi.
Milanzi alieleza kuwa Oktoba 12 mwaka jana, alikuwa katika eneo lake la kazi lilopakana na Markas kuanzia asubuhi  na kwamba alipoajiriwa alikuwa ameukuta ukuta ambao hivi sasa haupo  na kwamba ukuta uliopo sasa ni mpya  na kwamba ukuta ule wa zamani ulivunjwa na umati ule uliovamia siku hiyo.
 “Ilipofika saa saba mchana ya Oktoba 12 mwaka jana,baada ya Sala ya  Ijumaa, niliona  umati mkubwa  sana na nikaona mbao nilizokuwa nazilinda zikichukuliwa na umati ule na na zikavushwa kupelekwa kwenye kiwancha  upande wa pili wa Markas ….baada ya muda nikaona umati huo unaingia kwenye mpaka ule uliokuwa uliokuwa ukijengwa kwaajili ya kutenganisha marks na msikiti  na kuanza kuvunja sehemu ndogo iliyokuwa imeezekwa kwa mabati;
“Baada ya kuvunja wakaingia eneo niliokuwa nalinda  na kuanza kubeba matofali  na kwenda nayo upande wa pili wa eneo la Markas  na nilipomjulisha bosi wangu Seif kuhusu hali hiyo, akanitaka niwe mtulivu  kwani anafanya mawasiliano na vyombo vya usalama na matofali yale ni mali ya Suleiman”alidai Milanzi.
Aidha alidai watu toka katika umati ule ambao hakuweza kuwatambua waliwafuata wao na kuanza tuuliza kama wao ndiyo wenye mali ya kiwanja cha Markas ,akawajibu kuwa wao ni walinzi mwenye mali ni Suleiman  na kwamba wale watu sita ambao walikuwa wamefuka vipaza sauti katike eneo hilo walijitambulisha kwao kuwa wao ni waislamu  na kwamba wamekuja pale kwaajili ya kuja kuhani  eneo lao  na waliwataka walinzi hao wakamweleze bosi wao kuwa akamtafute aliyemuuzia kiwanja hicho amrudishie fedha zake na kwamba umati ule umekuja kuchukua eneo  lao ambalo ni mali ya waislamu.
“Mheshimiwa hakimu umati ule ulichukua matofali yale  na kuyapeleka  eneo la Markas na umati ule uliendelea kudumu katika kiwanja hicho toka Oktoba 12 hadi 16 mwaka jana alfajiri ambapo polisi walikuja kuwakamata  na wakati wameweka kambi kwa siku hizo zote katika kiwanja hicho,umati huo ulikuwa umefunga vipaza sauti katika eneo hilo ambapo wakulikuwa wakitangaza  eneo lile lilokuwa limetobolewa kwaajili ya kujenga ukuta wa kutenganisha msikiti na markas lizibwe kwa matofali yale yale waliyoyakuta pale  na wakavunja na kibanda cha mabati”alidai Milanzi.
Kwa upande wake hakimu Nongwa aliairisha kesi hiyo hadi  Februali 14 itakapokuja kwaajili ya kutajwa na kusema kuwa siku hiyo aletwe Ponda na mshtakiwa wa tano tu, Mkadamu ndiyo waletwe mahakamani kwasababu wanaishi gerezani na kwamba washtakiwa waliosalia wasije mahakamani kwasababu wanadhamana na akasema kesi hiyo itakuja tena Februali 18,25,27 na 28 mwaka huu, kwaajili ya shahidi wa nane wa upande wa jamhuri kuanza kutoa ushahidi wake, na kuamuru Ponda na Mkadamu warudishwe gerezani kwasababu Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Dk.Eliezer Feleshi bado hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana washtakiwa hao.
Hata hivyo jana hali ya usalama iliimalishwa kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na Januari 17 mwaka huu, kesi hiyo ilipokuja kwaajili ya kusikilizwa, kwani zaidi wafuasi wa Ponda 200 walikuwa wamefurika ndani ya viwanja vya mahakama hiyo na walijipanga katika viwanja hivyo wakisubiri basi la Jeshi la Magereza lilokuwa limembeba Ponda na Mkadamu lipite kwaajili ya kuwapeleka gereza la Segerea, ndipo umati huo ulianza kupaza sauti ya juu kwa kusema ‘Takbir   Allahwakbar,Takbir Allahwakbar’, huku wengine wakilisogelea basi alilokuwa amepanda Ponda.
“Nyie Polisi mmezidi sana, sasa kwa taarifa yenu kesho (leo) mjiandae kutuua sana kwa risasi, tunasema mjiandae kutuua kwa risasi…..serikali ya awamu ya nne ina wapendelea sana wakristo na inatugandamiza waslamu, tumechoka “walisikika wafuasi hao waliokuwa wamevalia kanzu na baraghashia wakisema.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Februali Mosi mwaka 2013. 

4 comments:

Anonymous said...



Heгe is my homeρage :: payday loan online
My website :: payday loan online

Anonymous said...



Нere is my hοmеpage payday loan,
Feel free to surf my web site ... payday loan online

Anonymous said...

Nice blog here! Also your site loads up fast! What web host
are you using? Can I get your affiliate link to your host?
I wish my site loaded up as fast as yours lol

Also visit my site How to get rid of static cling
My web page How to get rid of static electricity

Anonymous said...

I am in fact delighted to read this blog posts which carries plenty of valuable
information, thanks for providing these kinds of data.

Here is my web site ... Biotin for Hair Growth Reviews
Also see my page :: Biotin for Hair Growth Reviews

Powered by Blogger.