Header Ads

GULAM DEWJI ABURUZWA KORTINI

Na Happiness Katabazi

SHIRIKA la Nyumba la Taifa(NHC), imeiburuza katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi ,Bodi ya Udhamini ya Federation of Khoja Ithna-Asheri Jamaats of Afrika na mfanyabiashara maafuru nchini Gulambhai Dewji wakiomba mahakama hiyo itamke jengo lililopo kitalu Na.39 mtaa wa Chuma-Chang’ombe jijini hapa ni mali halali ya shirika hilo na si la wadaiwa hao.

Kesi hiyo ya madai namba 23 ya mwaka huu na tayari imeishapangwa kuanza kusikilizwa mbele ya Jaji Chingilwe Machi 24 mwaka huu, mlalamikaji(NHC) anatetewa na wakili wa kujitegemea Jerome Msemwa na tayari mahakama hiyo imeishatoa hati za wadaiwa kuitwa mahakamani siku hiyo.

Kwa mujibu wa hati ya madai ambayo gazeti hili inayo nakala yake, mlalamikaji ambaye amefungua kesi hiyo chini ya hati ya hati ya dharula , na Mwanasheria wa Shirika hilo la Nyumba nchini, Martin Mdoe ndiye amekula kiapo kwaniaba ya Mkurugenzi Mkuu wa (NHC), anaiomba mahakama hiyo itamke kuwa jengo hilo ambalo lina thamani ya zaidi ya bilioni mbili ni mali ya shirika hilo.

Shirika hilo linadai jengo hilo ni mali yake na si mali ya mdaiwa wa kwanza kama mdaiwa huyo wa pili alivyojiingiza kwenye umiliki wa jengo hilo Oktoba 23 mwaka jana kwa njia ya udanganyifu na kughushi.

“Tunaiomba mahakama hii itamke wadaiwa hao siyo wamiliki halali wa jengo lile kwani hata mwaka 1971 serikali ilipotoa amri ya kuyataifisha majengo hapa nchini jengo hilo lilikuwa likimilikiwa na Albai Punja Khoja Shia Education Trust na hata lilipotaifishwa mmiliki huyo Albai Punja Khoja Shia Education Trust ndiyo April 27 mwaka 1992 ndiyo aliyeandika barua kwa rais wa awamu ya pili, All Hassan Mwinyi awarejeshee jengo hilo;

“Lakini ilipofika Januari 1996 serikali ya Tanzania kupitia aliyekuwa Waziri Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi , alibatirisha agizo la rais Mwinyi lilokuwa limekubali maombi ya baadhi ya waliokuwa wamiliki wa majengo hayo yaliyotaifishwa na serikali na kuongeza kuwa mdaiwa wa kwanza hakuwai kuwa miongoni mwa waliopeleka maombi kwa Mwinyi wala wizara ya Ardhi yakuomba arejeshewe jengo kwasababu hakuwahi kuwa mmiliki wa jengo hilo”alidai Msemwa.

Aidha alidai kuwa Oktoba 23 mwaka jana , mdaiwa wa kwanza alikwenda wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi kubadilisha hati inayoonyesha jengo hilo ni mali yake na mdaiwa huyo akamteua mdaiwa wa pili Gulambahi Dewji kwa barua ya Agosti 4 ya mwaka jana ambayo imesainiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini ya Federation of KLhoja Ithna-Asheri Jamaats of Afrika, Anwaralui Dharamsi ya kumtoa kwenye jengo hilo mpangaji ambaye alikuwa amepangishwa kihalali na NHC, ambaye ni M/S FAZAL&CO.LTD agizo ambalo mdaiwa wa pili mdaiwa wa pili alilitekeleza kwa vitendo.

Aidha Msemwa katika hati hiyo ya madai anaeleza kuwa sababu nyingine iliyosababisha mteja wake kuamua kuwaburuza mahakamani wadaiwa hao ni kwamba mdaiwa wa kwanza ambayo ni bodi ya wadhamini ni kigeni na kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Tanzania inakataza kampuni ya kigeni kumiliki ardhi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Machi 17 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.