Header Ads

SHAHIDI:DECI WALIKUWA WAKIWEKA FEDHA UVUNGUNI

Na Happiness Katabazi

MRAKIBU wa Polisi(SP) Suleiman Nyakulinga ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa katika upelelezi wao Jeshi la polisi liligundua viongozi wa matawi ya mikoani ya Taasisi ya Entrepreneurship for Community Initiative(DECI)walikuwa wanaifadhi fedha za wananchama uvunguni na kwenye droo za ofisi badala ya benki.

SP-Nyakulinga ambaye ni mpelelezi toka Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ni shahidi wa sita wa upande wa Jamhuri na aliyatoa maelezo hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Stewart Sanga wakati akihojiwa na mawakili wa utetezi Onesmo Kyauke na Hudson Ndusyepo.

Shahidi huyo alieleza mahakama kuwa Juni 2009, Jeshi la Polisi ndiyo serikali ilizikamata akaunti zote za DECI na hapo ndipo jeshi la polisi lilipanza uchunguzi wake kwa matawi ya DECI kote mikoani na kubaini kuwa matawi ya mikoani yalikuwa yakiifadhi fedha hizo za mchezo haramu wa upatu zilikuwa zikiifadhiwa uvunguni na kwenye droo za ofisi na kuongeza kuwa pia uchungizi wao ulibaini kuwa DECI haikuwa na leseni ya biashara hivyo haikuwa imealalishwa kama kampuni.

Akijibu swali la wakili wa utetezi Kyauke lilitaka kufahamu ni kwanini polisi walifikia uamuzi wa kuwakamata washtakiwa hao badala ya kuishtaki kampuni hiyo , shahidi huyo alidai kuwa yeye ndiye aliyemhoji mshtakiwa wa kwanza na wapili na kwamba hawajawahi kumweleza kwamba ni mawakala wa DECI hivyo ndiyo maana polisi wakamaamua kuwakamata.

Aidha alipotakiwa ajibu swali ni kabla ya polisi kuzifunga akaunti za DECI, kuna mwanachama wa DECI alishafika polisi kulalamika kwamba wamedhulumia fedha zao taasisi hiyo, shahidi huyo alidai kuwa hawakuwai kupokea malalamiko ya wanachama wa taasisi hiyo kudhulumiwa fedha zao.Kesi hiyo iliairishwa hadi leo ambapo shahidi wa saba wa upande wa Jamhuri ataanza kutoa ushahidi wake.

Mwaka 2009, washtakiwa katika kesi hiyo ni Jackson Mtares, Dominic Kisendi, Timotheo ole Loitgimnye, Samuel Mtares, Arbogast Kipilimba na Samuel Mtalis,walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza na Jamhuri ilidai kuwa washtakiwa wanamakosa ya kuendesha na kusimamia mradi wa upatu kinyume na sheria pamoja na kupokea amana za umma bila leseni na Na upande wa Jamhuri unawakiliwa na Mwanasheria wa Kanda ya Dar es Salaam, Justus Mulokozi na Prosper Mwangamila.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Machi 18 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.