Header Ads

MSIBA WAMKWAMISHA MURRO ASIJITETE


Na Happiness Katabazi
ALIYEKUWA Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa(TBC1) Jerry Murro jana alishindwa kupanda kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuanza kujitetea katika ya kula njama, kushawsishi na kuomba rushwa ya Sh milioni 10,kwasababu amesafirisha msiba wa baba yake mdogo mkoani Kilimanjaro.


Mbele ya Hakimu Mkazi Gabriel Mirumbe Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka,Stanslaus Boniface aliikumbusha mahakama hiyo kwamba kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya Murro na wenzake kuanza kujitetea kutokana na uamuzi wa mahakama hiyo uliotolewa Machi 8 mwaka huu,ambao uliowaona washtakiwa wote wana kesi ya kujibu na kwamba kwa upande wa Jamhuri upo tayari kwaajili ya kusilikiza utetezi wa washtakiwa.

Baada ya Boniface kuikumbusha mahakama, wakili wa kujitegemea Richrad Rweyongeza aliwasilisha ombi la kuomba kesi hiyo iairishwe kwasababu Murro hayupo mahakamani amekwenda mkoani Kilimanjaro kwaajili ya kumzika baba yake mdogo na kwamba mshtakiwa huyo alileta ombi la udhuru huo juzi.

Hata hivyo ombi hilo lilikubaliwa na Hakimu Mirumbe ambapo aliairisha kesi hiyo Mei 2-3 mwaka huu, ambapo washtakiwa hao wataanza kujitetea mfululizo kwa siku hizo mbili.
Mbali na Murro, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Edmund Kapama na Deogratius Mugasa ambao wanadaiwa kuwa Februali milioni 10 kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo , Michael Karoli Wage.Kati ya mashtaka matatu yaliyofunguliwa dhidi ya yao,Murro anakabiliwa na mashtaka mawili.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Machi 30 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.