Header Ads

MGIMWA ATAKA KUTUNISHA MFUKO WA JIMBO

Na Happiness Katabazi

MBUNGE wa Mufindi Kaskazini Mahamoud Mgimwa (CCM), amewataka wananchi wa jimbo wanaoshi jijini Dar es Salaam na Pwani kushiriki kuchangia mfuko wa maendeleo wa jimbo hilo.


Mgimwa alitoa rai hiyo juzi katika mkutano wake na wananchi wa jimbo hilo wanaoishi mkoani hapa Dar es Salaam na Pwani uliofanyika katika Hoteli ya Travetine, alisema lengo la kuwashirikisha wananchi hao ili waweze kuchangia katika mfuko huo ni kutaka kuleta maendeleo.

“Wananchi wa Mufindi Kaskazini siyo tu wanaishi jimboni humo tu wengine ndiyo kama nyie mmetawanyika mikoa mingi ya Tanzania kutokana na majukumu ya kikazi... sasa nimewaita hapa ili niwashirikishe katika uanzishwaji wa mfuko huo ambao wananchi mkihamasika kuuchangia ni wazi jimbo letu litapata maendeleo kwa kasi kwani sio lazima tusubiri serikali ituletee hata sisi wananchi kwa michango yetu tunaweza kuleta maendeleo,” alisema Mgimwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Machi 8 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.