Header Ads

KESI YA NG'UMBI Vs MYIKA YAPIGWA KALENDA

Na Happiness Katabazi

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya (CHADEMA), John Mnyika jana aliiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam impatie muda kwa kujibu hati ya kiapo ya mlalamikaji katika kesi ya kupinga ubunge wake iliyofunguliwa dhidi yake na aliyekuwa mgombea mwenzake kupitia (CCM), Hawa Ng’umbi kwasabu mdaiwa huyo hakuwa amempatia hati ya madai ya kesi hiyo pamoja na ombi la kuomba kupunguziwa ada ya kuendesha kesi hiyo.


Katika kesi hiyo Na. 107/2010 ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka jana ambayo yalimtangaza Mnyika kuwa ndiye mshindi.Hawa Ng’umbi ambaye Mkuu wa Wilaya ya Bukombe ambaye anatetewa na wakili wa kujitegemea Issa Maige anamshtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mnyika na aliyekuwa Msimamizi wa Jimbo la Ubungo kwamba taratibu za uchaguzi zilikiukwa na kwamba mdaiwa wa kwanza na wa tatu walishindwa kutimiza wajibu kikamilifu.

Ombi hilo lilitolewa jana na wakili wa Mnyika, Edson Mbogoro mbele ya Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,Amir Msumi ambapo alidai kuwa hadi kufikia jana mteja wake ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo hakuwa amepatia hati ya kiapo na ombi la mlalamikaji la kuiomba mahakama impunguzie kiwango cha ada ya kuendesha kesi hiyo hivyo anaomba mahakama mahakama imwamuru mlalamikaji ampatie hati hiyo ya kiapo na ombi hilo ili aweze kujibu.

Msajili Msumi alikubaliana na ombi hilo na akamkata Mnyika awasilishe majibu ya hati hiyo ya kiapo na ombi la mlalamikaji la kuomba apunguziwe ada ya kesi Aprili 4 mwaka huu na akaiarisha kesi hiyo Mei 5 mwaka huu, kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Hata hivyo Msajili Msumi alisema licha ya Mnyika kutokabidhiwa nyaraka hizo tayari wadaiwa wenzake katika kesi hiyo ambayo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi Uchaguzi wa Jimbo la Ubungo tayari walishakabidhiwa nyaraka na mlalamikaji Hawa Ng’umbi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bukombe.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Machi 31 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.