Header Ads

MAHALU AMKATAA JAJI

Na Happiness Katabazi
ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Grace Martin ambao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ya zaidi ya Euro milioni mbili, jana walimwomba Jaji Sivangilwa Mwangesi ambaye anaendesha kesi hiyo hajitoe kwasababu amekuwa akikiusha sheria kwa makusudi kwasababu ya malengo anayoyajua yeye.

Ombi hilo limetolewa jana na mawakili wa washtakiwa haoMabere Marando aliyekuwa akisaidiwa na Beatusi Malima na Alex Mgongolwa ambapo kwakuanza waliiumbukusha mahakama hiyo kuwa wanafahamu kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya jaja huyo kupanga tarehe ya washtakiwa hao kuanza kujitetea.
Wakili Marando alidai kuwa wana sababu sita ambazo wamwomba Jaji Mwangesi ajitoe ambapo aliitaja sababu kwanza ni kwamba upande wa utetezi ulishatoa mahakamani hapo Ansard ya bunge ya mwaka 2004 iliyomnukuu aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje katika serikali ya awamu ya tatu ambaye kwasasa ni rais Jakaya Kikwete akieleza bunge kuwa manunuzi ya jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Italia ulikidhi matakwa ya Sheria ya manunuzi ya umma na kwamba hakukuwa na wizi katika ununuzi huo lakini jaji huyo akuzingatia ansard hiyo.

Sababu ya pili ni kwamba Mwangesi kuwa alivunja sheria ya Ushahidi ya mwaka 2002 wakati akipokea ushahidi wa shahidi wa jamhuri kwa njia ya video na kwamba shahidi huyo ambaye ni wakili wa Italia alitoa ushahidi wake katika kesi hiyo inayoendeshwa hapa nchini akiwa nchini Italia, jambo kitendo ambacho kinakiuka sheria hiyo ya ushahidi.
“Wewe Jaji Mwangesi ulipindisha makusudi sheria hiyo na kuchukua ushahidi wa shahidi huyo kwa njia ya video wakati sheria ya nchi hii inakataza na ndiyo maana hivi sasa serikali inapeleka muswaada bungeni wa kuifanyia marekebisho sheria ya sasa hili sheria hiyo mpya ikitungwa ndiyo itakuwa ikiruhusu mahakama kuchukua ushahidi kwa njia ya video”alidai Marando.

Sababu ya tatu ya kumtaka ajitoe ni kwamba tangu mapema upande wa washtakiwa waliuomba upande wa Jamhuri uwatajie mlalamikaji wa kesi hiyo na upande wa Jamhuri ulishawahi kuieleza mahakama hiyo kuwa kesi hiyo haina mlalamikaji lakini jaji huyo alishtusha na kauli hiyo ya Jamhuri na akaiarisha kesi na kuwautaka upande wa jamhuri ukamlete mlalamikaji na mwisho wa siku jamhuri ilienda kuleta nakala ya nusu kurasa ya maelezo ya mlalamikaji ambaye ni akisa wa TAKUKURU,na mbaya zaidi jamhuri hadi inafunga kesi yao hakuweza kumleta mlalamikaji huyo kutoa ushahidi wake mahakamani.

“Kwa hiyo sisi upande wa utetezi tunasema kwa kitendo cha wewe Jaji Mwangesi kuung’ang’ania upande wa Jamhuri walete mlalamikaji wa kesi hiyo huku upande wa Jamhuri ulishawahi kumleleza kuwa kesi hiyo haina mlalamikaji kimetunyima fursa sisi kuwasilisha ombi la kutaka kesi hiyo ifutwe kwasababu ilikuwa haina mlalamikaji”alidai Marando.
Sababu ya nne ni kwamba jaji huyo aliunyima haki upande utetezi wa kuwasilisha majumuisho ya kuwaona hawana kesi ya kujibu pale jaji huyo kwa malengo yake anayoyajua yeye siku Jamhuri ilipofunga kesi yake na ndipo siku hiyo hiyo akatoa uamuzi wa kuwaona washtakiwa wanakesi ya kujibu.
“Sababu ya tano ya kukataa jaji wewe ni kwamba wewe unasikiliza kesi hii kama hakimu wa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwasababu mahakama zote zina mipaka ya ardhi ya kufanyakazi zake isipokuwa Jaji Mkuu anaweza kutoa kibali maalum kwa mahakama husika kusikiliza kesi iliyo nje ya mamlaka yake … lakini wewe mheshimiwa jaji hukupata kibali cha Jaji Mkuu na ukadiriki kupokea ushahidi wa shahidi wa Jamhuri aliyekuwa nchini Italia kwa njia ya video jambo ambalo tunaliona ulikiuka makusudi sheria za nchi kwa malengo yako binafsi.”alidai Marando.
Alitaja sababu ya sita ni kwamba alikiuka kwa makusudi sheria za Tanzania kwakukubali kwake kupokea nakala kivuli ya mkataba wa mauzo ya ununuzi wa jengo la Ubalozi wa Italia kama kielelezo toka kwa shahidi wa Jamhuri ambaye ni wakili wa nchini italia ambaye alikuja hapa nchini kutoa ushahidi ambapo shahidi huyo aliambia mahakama kuwa kwa mujibu wa sheria za Italia hazimruhusu yeye kuutoa mkataba halisi na jaji huyo akakubaliana na hoja ya shahidi huyo wakati sheria za Tanzania zinakataza hilo na kwamba alikubali kupokea kielelezo hicho ambacho kiliandaliwa na shahidi huyo mwenyewe ambaye ni wakili huyo wa Italia wakati sheria za Tanzania zinakataza mkataba unaondaliwa na mwanasheria husika zisibitishwe na mwanasheria huyo huyo bali zikathibitishwe na mwanasheria mwingine.
Jaji Mwangesi badala ya kusikiliza hoja hizo aliairisha kesi hiyo hadi Jumatatu Machi 28 mwaka huu, ambapo atatoa uamuzi wa kujitoa au kutojitoa katika kesi hiyo.
Mapema mwaka 2006 ,Jamhuri alimfikisha Mahalu na Martin katika mahakama hiyo wakidai manunuzi ya jengo hilo hayakufuata sheria za manunuzi, na kwamba waliibia serikali kiasi hicho cha fedha kwaajili ya ununuzi wa jengo hilo.

Chanzo Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Machi 26 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.