Header Ads

MKENYA KORTINI KWA UTAKATISHAJI FEDHA



Na Happiness Katabazi

RAIA wa nchini Kenya Donibosco Ooga Bcha jana alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, akikabiliwa na makosa mawili likiwemo kosa la utakatishaji fedha haramu zenye thamani ya Sh.bilioni 7.9.

Wakili Mwandamizi wa Serikali Oswald Tibabyekomya mbele ya Hakimu Mkazi Emilius Mchauru alilitaja kosa la kwanza kuwa ni la kula njama kutenda kosa la  ambapo inadiwa kuwa kati ya Novemba 2009 na Agosti 2010 huko Nairobi nchini Kenya, Arusha na Dar es Salaam,mshitakiwa huyo alitenda kosa la utakashaji fedha haramu.

Wakili Tibabyekomya alilitaja kosa la pili kuwa ni la utakajishaji fedha zenye thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 4.9  sawa na Sh.bilioni 7.9  toka Nairobi kwenda Arusha kuja Dar es Salaam.
Na kwamba anadaiwa kuamisha kiasi hicho cha fedha kwa kutumia hundi yenye Na. 02J1036325000 inayomilikiwa na Moyale Prepious Germs Enterprices iliyopo benki ya CRDB  tawi la Meru mkoani Arusha.

“Na kisha anadiwa kuamisha kutoka katika Tawi hilo la Arusha  kuja Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam kwania ya kufanya  utaratibu  wa kuzitoa fedha hizo wakati akifahamu hundi hiyo ilikuwa imegushiwa “alidai wakili huyo na kudai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hata hivyo hakimu Mchauri alimtaka mshitakiwa huyo asijibu chochote  kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kwamba mahakama yenye mamlaka ya kuisikiliza ni Mahakama Kuu na akaiarisha kesi hiyo Aprili 18 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na akaamuru mshitakiwa apelekwe gerezani.
  
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Aprili 11 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.