Header Ads

WALIOFANYA FUJO KATIKA KITUO CHA POLISI KAWE KORTINI



Na Happiness Katabazi

WATU 12 jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kwa makosa nane yakiwemo makosa ya kuaribu vioo vya magari ambavyo ni vielelezo na kuwajeruhi kwa mawe askari polisi wa Kituo cha Polisi Kawe.

Mbele ya Hakimu Mkazi Geni Dudu wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka alimtaja mshitakiwa wa kwanza kuwa  Alex Kalinga na wenzake 12 ambapo miongoni mwao ni mwanamke mmoja aitwaye Eva Maheji.

Wakili Kweka alilitaja kosa la kwanza kuwa ni la kula njama kutenda kosa  kuwa Aprili 3 mwaka huko katika kituo cha Polisi Kawe alishitakiwa hao kwa pamoja walitenda kosa hilo.

Kweka alidai kosala pili ni kufanya mkusanyiko husio halali ikiwa ni kwa washitakiwa hao kutekeleza lengo moja ovu,walifanya mkusanyiko huo haramu ambayo ulisababisha kuvunjika kwa amani.

Kosa la tatu ni la kukaudi amri ya jeshi la polisi iliyokuwa ikiwataja watawanyike, kuwa Aprili 3 mwaka huu, katika eneo hilo la Kituo cha Polisi Kawe jeshi hilo lilitoa amri iliyowataka watawanyike lakini washitakiwa hao walikaidi.

Alilitaja shitaka la nne ,tano, sita ni mashumbulio ya kudhuru mwili kwamba siku hiyo washitakiwa waliwashambulia askari polisi waitwao  Felex kwa kumpiga na jiwe kifuani, na pia walimshambualia kwa kumpiga na jiwe usoni askari polisi aitwaye Harrison na askari polisi aitwaye  Aziz  walimpiga na jiwe kichwani.

Wakati shitaka la saba ni la kuharibu mali  ambapo siku hiyo washitakiwa hao walivunja kioo cha gari lenye namba za usajili Na. T 212  APS Toyota  Caridina chenye thamani ya Sh.400,000.

Kosa la nane ni washitakiwa waliaribu kioo cha gari lenye Na. T 646 AZN Isuzu  Troper chenye thamani ya Sh 400,000. Magari yote hayo yaliyoaribiwa ni vielelezo vya kesi mbalimbali ambayo yameifadhiwa katika Kituo hicho.

Hata hivyo washitakiwa wamekana mashitaka yote na wakili Kweka amedai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na akaomba mahakamaiangalie mazingira na uzito wa kesi  wakati inatoa dhamana na kwamba upande wa jamhuri  inaona kwasasa  suo wakati mwafaka  kwa mahakama hiyo kuwaoatia dhamana kwaajili ya usalama wao  kwaajili ya sababu za upelelezi wa kesi hiyo.

Kwa upande wao washitakiwa kila mmoja wao alikuwa akinyosha kidole juu, akiomba mahakama impatie dhamana.

Lakini hata hiyo Hakimu Dudu alisema mahakama yake inawanyima dhamana kwa muda  hadi mangira ya kiusalama yatakapotengamaa na akaiarisha kesi hiyo hadi Aprili 23 mwaka huu,itakapokuja kwaajili ya kutajwa na akaamuru washitakiwa wote wapelekwe gerezani.

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com, Aprili 10 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.