Header Ads

MAUJI,MAUAJI JAMANI

Watanzania huyu ni binadamu mwenzetu ambaye leo alfajiri ya kuamkia leo Aprili 20 amekutwa na mauti.Sisi wakazi wa Mtaa wa Sinza 'C' eneo la Ukuta wa Posta maarufu kama ukuta wa Kesi ya Abdallah Zombe, leo saa 11 alfajiri tulijikuta tukiamkia kuona mwili wa marehemu huyo ukivuja damu katikati ya barabara na ukiwa umelazwa chini baada ya kuua na watu wasiyojulikana.Nikiwa kama raia mwema na Mwandishi wa habari baada yakufika eneo hilo la tukio nilichofanya nikumpigia Simu mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Ilala,ACP-Duwani Nyanda na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP- Charles Kenyela kuwapa taarifa na kweli baada ya muda mchache waliwaagiza askari wao wakafika eneo la tukio na kuuchukua mwili huo ambao ulikuwa unavuja damu.Inasikitisha sana, na inaendelea kudhiirisha kuwa baadhi ya watanzania hivi sasa wamezidi kuwa na roho katili na hawana hofu ya mungu.(Picha na Happiness Katabazi)
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook:happy katabazi
Aprili 20 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.