Header Ads

CHE MUNDUGWAO ADAI ANATESEKA GEREZANI





Na Happiness Katabazi
UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya wizi wa paspoti inayomkabili msanii wa muziki wa asili nchini,  Chingwele Che Mundugwao na wenzake nane wanaokabiliwa na kesi ya wizi wa pasipoti 26 wamewasilisha taarifa ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa,inayoiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es salaam, iwaongezee siku 60 iliwaweze kuendelea kufanya upelelezi wao.
 
Mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo, wakili wa serikali Adolph Mkini aliwasilisha ombi hilo jana asubuhi ambapo alianza kwa kuikumbusha mahakama kuwa kesi hiyo ilikuja kwaajili ya kutajwa na kwamba upande wa jamhuri unaombi la kuwasilisha hati iliyoletwa na RCO ya kuiomba mahakama iwaongezee muda wa siku 60 kuanzia jana ili waweze kuendelea kufanya upelelezi wa kesi hiyo.
 
Baada ya Wakili Mkini kumaliza kuwasilisha ombi hilo, mshitakiwa Che Mundugwao alianza kuwasilisha kilio chake kuwa jela ni sehemu mbaya sana na kwamba wanavyozidi kukaa gerezani wanateseka pia wanaomba mahakama iwapatie dhamana kama ilivyomoatia dhamana Wilfred Lwakate wa Chadema na kwamba anaomba mahakama imruhusu wakili huyo wa serikali waongozane naye waende naye gerezani ili akashuhudie wanavyoteseka na maisha ya gerezani.
 
Hata hivyo Hakimu Fimbo alikubaliana na ombi hilo la RCO la kuomba waongezewe muda wa siku 60 na akasema mahakama yake haiwezi kutoa masharti ya dhamana kwa kesi hiyo  kwani ni MKurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi ndiye aliyewasilisha hati ya kuwafungia dhamana na moja ya sababu iliyotajwa na DPP ya kuwafungia dhamana ni  kwamba bado paspoti 22 hazijapatikana na kuwa bado washitakiwa wengine hawajakamatwa ili waje kuunganishwa kesi hiyo na ninawashauri washitakiwa mistake kufananisha mazingira ya kesi hii sawa na kesi nyingine kama ya Lwakatare, mazingira na mashitaka yanayowakabili nyie na Lwakatare ni tofauti..
“Kwa sababu hadi sasa DPP bado hajaiondoa hiyo hati yake ya kuwafungia nyie washitakiwa dhamana, mahakama yangu kisheria imefungwa mikono haiwezi kuwapatia dhamana hadi pale siku DPP atakapoamua kuindoa hati yake hivyo naamuru mrejeshwe rumande hadi Agosti 19 mwaka huu, kesi hii itakapokuja kwaajili ya kutajwa’alisema Hakimu Fimbo.
 
Mbali na Che Mundugwao washitakiwa wengine ni wahudumu wa Idara ya uhamiaji Adam Athuman na Abdallah Salehe ,  Rajab Momba na Haji Mshamu
Raia wa Uingereza Ahsan Iqbal au Ali Patel, Ofisa  Ugavi wa  Idara ya Uhamiaji Shemweta Kiluwasha, Injinia Keneth Pius wa Kikosi  cha Zimamoto na Uokoaji na mfanyabiashara Ally Jabir.
 
 Juni 3 mwaka huu, Chemundugwao na wenzake walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo wakikabiliwa na makosa mbalimbali yakiwemo kosa la wizi wa paspoti 26, ambapo hata hivyo DPP aliwasilisha hati ya kuwafungia dhamana ambapo hadi sasa wapo gerezani.
 
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Agosti 6 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.