Header Ads

ALEX MASSAWE AFUNGULIA KESI YA KUGHUSHI









*Mahakama yaamuru arejeshwe Tanzania

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,imetoa hati ya kukamatwa na kurejeshwa nchini  mfanyabiashara maarufu nchini Alex Siliyamala Massawe ili aje kukabiliana na kesi yake mpya ya kughushi nyaraka za umiliki wa ardhi na kutoa taarifa za uongo.
Amri hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Gene Dudu muda mfupi baada ya wakili Mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka kuwasilisha ombi hilo mahakamani na kuiarifu mahakama kuwa upande wa jamhuri umemfungulia   kesi Massawe na.150/2013 ya kughushi hati za umiliki wa ardhi na kutoa nyaraka za uongo mahakamani hapo na kumsomea mashashitaka Massawe ambaye anashikiliwa na Askari wa Interpol Dubai bila ya Massawe kuwepo mahakamani hapo .
Hakimu Dudu alisema anakubaliana na ombi hilo la wakili Kweka na kwamba mahakama yake imetoa amri ya kukamatwa kwa Masawe kokote alipo na arejeshwe nchini ili aje akabiliane na kesi yake hiyo mpya iliyofunguliwa mahakamani hapo.
Aidha Hakimu Dudu alisema pia anakubaliana na ombi la wakili Kweka lilokuwa linaiomba mahakama hiyo itamke majina sahihi yanayotumiwa na Massawe  hata kama  kule Dubai anakoshikiliwa na  askari wa Interpol anatumia majina mengi, ambapo hakimu Dudu alisema majina halali ya Massawe ni Alex Siliyamala Massawe ambayo ndiyo yaliyoandikwa kwenye hati ya mashitaka ya kesi hiyo Na.150 ya mwaka huu.
Hivi karibuni vyombo vya habari na Mkuu wa Kitengo cha Interpol cha Jeshi la Polisi hapa nchini , Babile alithibitishia vyombo vya habari kuwa Massawe amekamatwa na askari wa Interol huko Dubai kwa tuhuma mbalimbali.


Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Agosti 24 mwaka 2013

No comments:

Powered by Blogger.