Header Ads

JELA MIAKA MITANO KWA KUIBA KWENYE AKAUNTI YA JESHI LA POLISI

 
 
Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemhukumu Afisa wa Jeshi la Polisi  Edna Kadogo na wenzake kifungo cha miaka mitano jela baada ya kuwakuta na hatia ya makosa ya kula njama na kuibia Benki ya NMB jumla ya Sh. Milioni 330.
 
Mbali Edna wengine waliotiwa hatiani katika kesi hiyo iliyokuwa na jumla ya washitakiwa tisa ni Adelaida  Lwekoramu,
  na Joshua Joshua Aseno Onditi Joshua Aseno Onditi  washitakiwa wengine sita kuachiriwa huru.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Gene Dudu ambaye alianza kwa kuikumbusha mahakama kuwa katika jitihada za kuthibitisha kesi yao upande wa jamhuri uliokuwa ukiwakilishwa na wakili wa serikali  na mahakama hiyo baada ya kuona upande wa jamhuri umeshindwa kuthibitisha kesi yake dhidi ya washitakiwa hao sita ambao ni Vedastus Limbu Mafuru,
Kennedy Agumba Achayo
Luciana Vedastus Limbu,
Agnes Robert Maro,
Mkika Gideon Nyasebwa na.
Amos Kabisi Hangaya,
Vedastus Limbu Mafuru,
Kennedy Agumba Achayo
Luciana Vedastus Limbu,
Agnes Robert Maro,
Mkika Gideon Nyasebwa na.
Amos Kabisi Hangaya,
 ila imeweza kuthibitisha kesi yake dhidi ya washitakiwa hao watatu na washitakiwa wote walikuwa wakitetewa na mawakili wa kujitegemea Karegero Karegero na Ambokile Mwakaje.
 
Hakimu Dudu alisema kesi hiyo ilikuwa na jumla ya mashahidi 21 wa upande wa jamhuri na mashahidi 10 wa upande wa utetezi mashitaka matatu ambayo ni kula njama, kughushi na wizi wa sh.milioni 330 ambapo  ambapo alisema shitaka la kwanza la kula njama na shitaka la tatu la wizi wa kiasi hicho cha fedha upande wa jamhuru umeweza kuyathibitisha na kosa la kughushi, limeshindwa kuthibitika.
 
“Kwa sababu hiyo mahakama hii ina wahukumu washitakiwa hao watatu  katika kosa la kwanza la kula njama kwenda jela mwaka mmoja, na katika kosa la tatu la wizi watakwenda jela miaka mitano ili iwe fundisho kwa watu wengine kwani makosa ya wizi wa fedha kwa njia ya mtandao yameanza kushamiri na kwamba anaukataa utetezi wa mwisho wa washitakiwa hao watatu ambao waliomba wapunguziwe adhabu kwasababu wanafamili kubwa zinategemea na kwamba sababu hiyo haiwezi kuishawishi mahakama iwapunguzie adhabu kwasababu mimi binafsi naamini kama mtu anafamilia kubwa inamtegemea basi mtu huyo anapaswa aepuke kutenda makosa ya jinai”alisema Hakimu Dudu.
Mwaka 2010 ilidaiwa na upande wa jamhuri kuwa washitakiwa wanaokabiliwa na kesi hiyo ya Na. 40/2010 kuwa wanakabiliwa na kosa la kula njama, kughushi na wizi  wa kiasi hicho cha fedha   kwenye akaunti inayomilikiwa na Jeshi la Polisi inayotambulika kwa jina la Police Retention Collection Account No. 2011000015 kwenye benki ya NMB Meatu.
  
Washtakiwa baadhi yao walikuwa wafanyakazi wa NMB Meatu Tawi la Mwanhuzi na wengine walikuw wafanyabiashara.
 

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com, Jumanne ,Agosti 6 mwaka 2013



No comments:

Powered by Blogger.