Header Ads

PONDA ATOLEWA WODINI,APELEKWA GEREZA LA SEGEREA


Na Happiness Katabazi
JESHI la Polisi na Jeshi la Magereza yamemwondoa  hospitalini kimyakimya Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam, Sheikh Ponda Isa Ponda, na kumpeleka katika gereza la Segerea bila ndugu zake kuwa na taarifa.
Wakili  wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda (54) ambaye kwa sasa anakabiliwa na kesi mpya ya kufanya uchochezi katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Nassor Jumaa, ameliambia gazeti hili jana saa saba mchana nje ya viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar  es Salaam, kuwa amesikitishwa na hatua  ya vyombo vya dola jana asubuhi kumuondoa Ponda aliyekuwa  amelazwa katika wodi ya Kitengo  cha Taasisi ya Tiba  ya Mifupa  na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu(MOI)  alikokuwa akipatiwa matibabu na kisha kumwamishia katika gereza la Segerea.
Wakili Jumaa alisema amesikitisha na kitendo hicho kwani hakimu Hellen Riwa juzi muda mfupi baada ya wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka kumaliza kumsomea shitaka Ponda, hakimu Liwa alitoa amri ya Ponda aendelee kukaa chini ya ulinzi lakini cha kushangaza leo(jana),wanausalama wamemto wodi na kumpeleka katika gereza la Segerea na kwamba atalazimika kurudishwa tena mahakamani siku kesi yake itakapojatwa Agosti 28 mwaka huu, ambapo upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
“Kwa kweli kitendo hicho kime nisikitisha na kunishitua sana ….ila tunatafakari ni hatua gani za kisheria tutazichukua huko siku za usoni’alisema wakili Jumaa.
Hata hivyo  baadhi ya maofisa wa Jeshi la Magereza walilithibitishia gazeti hili kuwa Ponda amepelekwa rumande ya gereza la Segerea na kudai kuwa wao walikua ni miongoni mwa waliotumwa kwenda kumtoa wodini mshitakiwa huyo(Ponda), na kisha kiumpeleka gereza la Segerea.
Agosti 14 mwaka huu, saa kumi jioni Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliamia katika wodi hiyo ya MOI na wakili wa serikali Tumaini Kweka alimsomea shitaka Ponda ambaye anakabiliwa na kesi hiyo ya Jinai Na.144 ya mwaka huu.
Wakili Kweka alidai mshitakiwa huyo anakabiliwa na kosa moja ambalo ni uchochezi kuwa Juni 2  hadi Agosti 11 mwaka huu, katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  akijifanya yeye ni Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania,  aliwashawishi waumini wake katika maeneo hayo kutenda makosa ya jinai, ikiwemo kosa la  kutoa lugha  ya kudhalilisha  dhidi ya viongozi wa serikali . kutoa maneno  ambayo yalikuwa na lengo ya kuamsha hisia na mawazo mabaya ya kidini  na aliwashawishi  wafuasi wake kufanya  mikusanyiko,maandamano haramu mkinyume na kifungu cha  390 na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002.
Baada ya wakili Kweka kumaliza kumsomea shitaka hilo,hakimu Riwa alitoa amri iliyotaka Ponda aendelee kukaa chini ya ulinzi wa vyombo vya ulinzi.
Mei 9 mwaka huu, aliyekuwa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Victoria Nongwa alimfunga Ponda kifungo cha mwaka  mmoja jela baada ya kumkuta na hatia katika kosa moja kati ya matano yaliyokuwa yakimkabilia mbapo kosa alilomtia nalo hatiani ni kosa la kuingia kwa jinai kinyume na kifungu cha 85 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, katika kiwanja cha Ch’angombe Marks.
Katika hukumu yake Hakimu Nongwa alisema anamfunga kifungo cha nje kwa mwaka mmoja, ila wakati Ponda akitumikia adhabu hiyo anatakiwa asitende makosa.
Oktoba 18 mwaka jana, Ponda na wenzie 49 walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza wakikabiliwa na makosa matano, kosa la kwanza ni la kula njama, kujimilikisha mali, kuingia kwa jinai katika kiwanja cha Chan’ombe Markas,wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh. Milioni 59 na kosa la uchochezi ambapo katika kesi hiyo Jamhuri ilikuwa ikiwakilishwa na serikali Tumaini Kweka na hakimu Nongwa akitoa hukumu yake alisema anawaachiria huru washitakiwa 49  kwasababu jamhuri wameshindwa kuthibitisha kesi dhidi yao na kwamba anamtia hatiani Ponda kwa kosa moja tu  la kuingia kwa jinai na kwamba na anamuachiria huru katika makosa manne yaliyosalia kwasababu pia jamhuri ilishindwa kuthibitisha mashitaka hayo dhidi ya Ponda.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Agosti 16 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.