Header Ads

MHARIRI KORTINI KWA TUHUMA ZA RUSHWA

 
Na Happiness Katabazi
MHARIRI wa Habari wa  Gazeti la Maua linalotolewa na kampuni ya Hamkani Publisher Company Limited, Ibrahim Katemi Kadiro (36) jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam, akikabiliwa na makosa mawili ya kuomba na kupokea rushwa ya Dola za Kimarekani 6,700.
 
Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Leonard Swai mbele ya Hakimu Janeth Kaluyenda alidai mshitakiwa ana kabiliwa na jumla ya makosa mawili.
Wakili Swai alilitaja kosa la kwanza kuwa ni kuomba rushwa na kuwa Julai 31 mwaka huu, katika Mtaa wa Samora  katika jengo la Habour View Tower , Kadiro akiwa ni wadhifa wa mhariri msaidizi  wa Hamkani Publisher  inayochapisha gazeti la Maua alimuomba rushwa sh.milioni 12 kutoka kwa  Costa Ginakopolous ili asichapishe habari mbaya  inayohusu biashara biashara zinazofanywa na kampuni ya Costa.
 
 Wakili Swai alilitaja kosa la pili kuwa ni la kupokea rushwa ambalo alilitenda  Agosti Mosi mwaka huu, ambapo alipokea dola za Kimarekani  6,700 kutoka kwa Costa  ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kampuni ya Thinany Entertaiment ili asiweze kuichapisha habari ya tuhuma zinazoikabili kampuni hiyo ambayo Costa ana mahusiano nayo ya kibiashara.
 
Hata hivyo mshitakiwa huyo alikana mashitaka na Hakimu Kaluyenda alisema makosa yanayomkabili mshitakiwa huyo yana dhamana kwa mujibu wa sheria ila hawezi kumpatia masharti ya dhamana kwa siku ya jana kwasababu yeye siyo hakimu aliyepangwa kusikilizwa kesi hiyo kwani hakimu aliyepangwa kusikiliza kesi hiyo ni Joyce Minde ambaye yupo nje ya ofisi na hivyo akaiarisha kesi hiyo hadi Agosti 16 mwaka huu, na akaamuru mshitakiwa apelekwe gerezani.
 
Wakati huo huo, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,  Ge
nu Dudu ameiarisha kesi ya  kujipatia kujipatia kofia,fulana zenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 74.9 kwa njia ya udanganyifu  inayomkabili waziri wa zamani na Kada wa Cha cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Arcado Ntagazwa na wenzake hadi Agosti 12,13 na 14.Kesi hiyo jana ilikuja kwaajili Ntagazwa kuanza kujitetea.
 
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Agosti 6 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.